• LinkedIn
  • Join Us on Google Plus!
  • Subcribe to Our RSS Feed

clean.sakamia.com Returning home to a house that’s clean, serene gives you a special and healthy feeling

Tuesday, May 23, 2023

10 FAIDA ZA KUSOMA KILA SIKU

4:49 AM // by Kalma // No comments

10 FAIDA ZA KUSOMA KILA SIKU

Lini ilikua mwisho kusoma kitabu,au gazeti,au maandiko yoyote?Je una tabia ya kusoma kila siku kwenye mitandao ya kijamii yaani Tweets,Facebook,au maelekezo katika vitu unavyotumia?Kama ni mmoja wapo ambaye husomi kila mara,kwa hali hiyo unakosa mambo mengi: kusoma kuna faida nyingi sana , na nyingine hizi zifuatazo hapo chini.

1. Kuistua akili

Wasomi wengi wameonyesha kwamba mara zote akili ikiwa inafanya kazi ina uwezekano mkubwa wa kulinda na ugonjwa wa Alzheimer na shida ya akili kitaalamu unaitwa Dementia, kufanya ubongo wako kua hai na huulinda usipunguze nguvu.Na hufanya kazi kama misuli mingine mwilini,akili inahitaji mazoezi ili iwe yenye nguvu na yenye afya.Ni sawa na kucheza michezo mingi kama mchezo wa bao unaochezwa kuanzia watu wawili, ni mchezo ambao husaidia kuifanya akili kuwa yenye nguvu.

2. Huondoa msongo wa mawazo 


Haijalishi una msongo wa mawazo wa kiasi gani inaweza kuwa kazini,katika mahusiano yako binafsi,au katika mambo ya maisha yako ya kila siku,la kufanya ni kutupilia mbali ikiwa utazubaa kwenye hadithi nzuri.Kitabuni au riwaya iloandikwa vizuri itakusafirisha kukupeleka kwingine kabisa,wakati hicho unachokisoma kitakufanya uwe katika hali iliomo humo kwa muda huo,huondoa wasiwasi na uoga na kitabu kitakupumzisha .

3. Maarifa 

Kila unachokisoma kinaleta habari mpya kichwani mwako,na huwezi jua kipi kitakuja mkononi mwako.Kuwa na maarifa mengi ,ndio kuwa na uwezo wa kupambana na changamoto zinazokukabili.
Kwa kuongezea zaidi,hiki ni chakula cha kukifikiria: ushawahi kukutana na hali ngumu,kumbuka yote hayo yanaweza yakapotea –kama hela ,kazi,nguvu,afya,lakini tisa kumi maarifa uliyokuwa nayo hayawezi potea na hubaki milele.

4. Upanuzi wa misamiati

Hii huendana na hiyo nukta ya hapo juu: unaposoma sana,ndivyo unajua misamiati mingi,na huwa ni maneno unayaotumia kila siku.Kujua misamiati mingi na kuongea kwa ufasaha ni msaada mkubwa katika taaluma yoyote,na tambua kwamba unaweza kuzungumza vizuri na ujasiri wote wa hali ya juu na itaongeza kujiamini na thamani yako kupanda pia.Itaongeza thamani ya kazi yako,kama wale wasomi wazuri,huongea vizuri,na wana maarifa ya kutosha katika mada tofauti tofauti huwa wanapata kukua na kujijenga haraka zaidi kuliko wale wenye misamiati kidogo na ujuzi wao udogo wa fasihi,utambuzi wa kisayansi,na matukio ya utandawazi.

Kusoma vitabu ni muhimu pia kwa kujua au kujifunza lugha mpya,kama kujua maneno yalokuwamo kwenye kurasa. Ambayo huongeza ujuzi wa kuyaongea na kuandika kwa ufasaha.

5. Huongeza kumbukumbu

Pindi unaposoma vitabu,unatakiwa kukumbuka wahusika,asili zao,matamanio yao,historia zao,na pia vitu tofauti tofauti vyenye mahusiano na wahusika kwa kila habari.Kwa mfumo wa kumbukumbu,lakini akili ni kipande cha maajabu ambacho huweza kukumbuka vitu na kukumbuka vitu hivyo vyote na hat mwisho wake vilipoishia. Ni jambo la ajabu ya kutosha,kila kumbukumbu mpya inayoingia katika akili hutengeneza ujuzi,na huzidishaukomavu wa akili,ambayo husaidiwa na mfumo wa muda mfupi wa kumbukumbu na kukomaza kukumbuka hizo hisia.Unaionaje hiyo? Imetulia!  

6. Uwezo wa uchambuzi sahihi

Hivi ushawahi kusoma vitabu vyenye hadithi za kusadikika,na ukapata suluhisho wewe mwenyewe kabla ya kumaliza kusoma? kama hivyo ndivyo,ulikuwa na uwezo wa kuchambua na kudadavua mawazo ukayafanyia kazi kwa kuandikamaelezo yote uliyoyapata na kutengeneza matumaini mapya.

Huo ni sawa na uwezo wa kuchambua ambao mikono yako imemiliki inapokuja haja ya uchambuzi. Kwanza kujua ulokiandika kipo sawa,kama wahusika walihusika vizuri, hadithi ilitiririka vizuri n.k. Ulishawahi pata nafasi ya kusimuliana kitabu na wengine,utakua na uwezo wa kuyachambua maoni yako kwa vizuri,kama uliutumia muda wako vizuri kufuatilia kila ulichokisoma.

7.Huongeza umakini wa uono wa maoni  

Katika  uchizi wa dunia ya mtandao,umakini unapatikana katika milioni ya muelekeo tofauti tofauti kwa wakati mmoja kama tunavyovifanyia kazi nyingi kwa kila siku. Kwa kila dakika tano ya maisha,wastani wa kila mtu hugawanya muda wake katika kafanya kazi,kuangalia barua pepe,kupiga soga yaani kuchat na watu zaidi ya mmoja,(kupitia gchat, skype, whatsaap n.k),macho yote kwenye twitter, kuangalia smartphone, na muingiliano baina na kati ya wafanyakazi wenzake. Hii aina ya tabia husababisha kuongezeka kiwango cha msongo wa mawazo,ambayo hupunguza uzalishaji wetu.

Pindi unaposoma kitabu,akili yako yote inakomaa na hadithi-na vingine vilobakia hupotea au  unavipuuza na utajidhatiti zaidi kujishughulisha na undani wa maelezo unayoyapata kutokea kwenye hadithi. Jaribu kusoma kwa 15-20 dakika kabla ya kazi(i.e asubuhi yako,kama unatumia usafiri wa wote),utashangaa kwa ugunduzi, maarifa na akili kuchangamka ambao uutakuwa umeupata ufikapo kazini.

8.Ujuzi wa kuandika vizuri  

Hii huwa mkono kwa mkono na uelewa mzuri kwa upana wake wa misamiati: Utaalam wa kuweka wazi,kazi nzuri ya maandishi huwa ni matokeo ya mwandishi mwenyewe,kama ugunduzi wa maanguko,mtirirriko,na aina ya uandishi wa baadhi ya waandishi,na utaalamu wa mbinu za uchoraji na utunzi wa waandishi tena wakufunzi waliopita, huwa ni matokeo kwa waandishi wameajifunza kutokea kwa kusoma kazi za wengine.

9. Utulivu

Kwa kuongezea kitabu kitakupa mapumziko au furaha ambayo inapatikana katika kusoma kitabu kizuri,na inawezekana somo unalolisoma likakupa faraja ,matumaini na utulivu wa amani ya nafsi. Kama kusoma vitabu vya imani,hushusha shinikizo la damu yaani blood pressure na hukupa upole aamani na utulivu,na pindi unaposoma vitabu vya sifa ya kutatua matatizo vinavyoonyesha jinsi ya kusaidia watu waliopata tabu katika hali fulani,navyo huleta maumivu ya kuumia.

10.Huburudisha bila ya gharama

Japokuwa wengi wetu tunapenda kununua vitabu na tunasoma na kuwa ndiokumbukumbu zetu za baadae,huweza vikawa bei iko juu. Na kwa kuwa na budget ndogo, au unakosa kabisa kiasi cha kukuwezesha kupata burudani ya vitabu ,unaweza tembelea maktaba ilokaribu na eneo lako au kupitia kwenye maduka na ukapata hata vitatu viwili. Maktaba zina vitabu vya kila aina ya somo uanalofikiria,na utakua unazunguka hifadhi yake utapata hata vipya pia,hautaepuka kuacha kusoma.

Kama itatokea utaishi eneo ambalo halina maktaba,au unaeza ukapata kwingine au hata kwa mtu mwingine kwa urahisi,maktaba nyingi zina vitabu vyake kwenye PDF au ePub kwahiyo unaweza soma kupitia mifumo hiyo,iPad,au compyuta yako.Pia kuna vyanzo vingi kwa njia ya mtandaoni ambapo huweza kupata vitabu vya bure, kwahiyo viwinde hivyo vipya na kisha usome!


Kuna utofauti wa tabia za kusoma kwa kila mtu duniani,na huenda ikawa ukaonja ladha tamu na nzuri
 katika fasihi ya waandishi,utenzi,magazeti ya mitindo,maandiko ya dini,vitabu vya vijana,jinsi ya kutoa msaada,mambo ya mitaani,au vitabu vya kimapenzi,hapo kitakuwepo kinachotaka kwenye akili yako na mawazo yako. Kaa pembeni na kompyuta yako kwa muda,fungua kurasa za vitabu,na ukonge moyo wako kwa wakati mwingine.  

usiache kutembelea blog yetu nayo inaburudisha kuisoma.






























Thursday, May 11, 2023

7 SABABU YA KUWA NA BUSTANI JIKONI

12:35 AM // by Kalma // No comments

 7 HIZI NI SABABU YA KUWA NA BUSTANI

 JIKONI

Kama ulikua unawaza mawazo ya kukuza viungo vyako mwenyewe,ni vizuri ukafanya hivyo! Chagua sehemu karibu na dirisha au balcony ya jikoni au ndani jikoni na upandishe mimea.Hutajutia! hizi ni sababu kwanini bustani za jikoni zitakushangaza.

1. Unapata viungo fresh pale unapohitaji

Mara nyingine unahitaji majani ya mint au basil,

unachuma tu hapo kwenye mmea wako na utaacha kwenda kununua. La kuongezea huhitajiki kununua fungu zima na kulihifadhi kwa mahitaji ya kutumia jani moja.2. Unajua haswa kile unachoweka kwenye chakula chako

Siku hizi,na hizi dawa zinazowekwa kuzuia wadudu,ni ngumu kujua kama chakula ni salama au laa.Kama unakuza au unazalisha mwenyewe,unajua kuwa ya kwamba na kuwa na uhakika kuwa chakula au mboga hizi ni salama na hazina dawa.3. Inakua kazi rahisi

Mimea haina gharama kubwa haswa pale inapokua imetulia,kikubwa kinachohitajika ni maji kidogo.Baada ya muda utatunza fedha yako ile na haitakuwa tena kwa ajili ya kununua  mboga mboga,na haswa pale unapohitaji vyakula vizuri na vilivyo fresh.

4. Unakua ni mwenye afya

Kama unazalisha na kuitunza  mimea kama tulsi na mint,unaweza kuwa unakula jani moja au majani mawili kila siku,au ukaweka kwenye chai ya asubuhi, au ukanogeshea mapishi yako.

Hivi viungo vina faida ya dawa za kutosha ambazo zimo kwa ajili ya kutibu magonjwakama vile changamoto ya upumuaji,inatunza afya ya meno,hutibu homa,asthma,changamoto ya mapafu,ugonjwa wa moyo na stress yaani msongo wa mawazo.

5. Unapata dozi ya utulivu ya kujituliza tena ya kiasili.

Bustani ni ina kazi ya kutuliza na kupunguza au kuondoa kiasi chamsongo wa mawazo na kusaidia  kuwa mwenye kupumzika.Kuzungukwa na mimea asili unatakiwa kuwa na hali ya muonekano mzuri wa afya ya akili, Pamoja na maandiko ya wasomi mengi kuona maajabu kwa ujumla.

6. Mimea hufukuza wadudu/mbuKama unachagua viungo haswa kwa kutulia,inaweza kufukuza mbu kwa kiwango kikubwa,inazuia na kupunguza kung’atwa na mbu na kinga dhidi ya dengue na malaria.

Mmea mzuri kwa kinga ya mbu ni marigold-weka mmea mmoja katika kila mmea wa viungo.Na rangi zake zitang’arisha nyumba yako pia!

7. Hali ya kushangaza

Unaweza kudharau wazo la kupanda mimea,lakini ukianza kukuza ya kwako mwenyewe,

Utajua haswa tunachomaanisha.Kila mpigo mmoja ,branch au maua yanayokuzwa itakupa hali ya kuridhika na kukupatia furaha wakati wote.



























Sunday, May 8, 2022

Ubunifu wa Matumizi ya Tea Bags

10:36 PM // by Kalma // No comments

 Ubunifu wa Matumizi ya Tea BagsUsitupe tea bags iliyotumika tena!

Tumia zaidi iliyotumika na usave hela na kupunguza taka.Kutibu macho na tea bags!Kuzuia  uvimbe wa chini ya macho kwa kutumia tea bags.Tumia kwa spa ujisikie vizuri ,itunze tea bags baada ya matumizi kwa dhumuni la kutumia tena. Furahia aromatherapy na athari zake za kujipumzisha .

Loweka miguu yakoChai ni kiburudisho chenye nguvu,huziba matundu na kuondoa ngozi chafu yenye mafuta.Kamua teabags iliypotumika na utumie mabaki ya mfano wa chai kwa kunawia miguu.

Chai nyeusi au black tea ni nzuri kwa kuondoa harufu mbaya miguuni, ambapo chai ya kijani hutuliza mwili nakuutia nguvu.

Umeungua?

Chai huponesha kuungua kwa jua, au kuchomwa na kiwembe au maumivu ya kuungua madogo madogo yatokanayo na kuunguzwa na sufuria au pasi.Hifadhi tea bags zilizotumika kwenye friji kwa muda wa wiki hadi mbili(njia nzuri na sahihi ya kuhifadhi kuweka kwenye mifuko yenye kufunga yaani air tight silicone bag,yenye unyevu),na utoe michache kwa ajili ya kutibu majeraha madogo kwenye ngozi yako.

Asidi za tannic ipatikanayo kwenye chai huzuia mtiririko wa damu kwenye cappilarries zako,inapambana na maumivu ya kuvimba au malenge lenge. Unaweza tumia tea bags kutibu kuvimba kulikosababishwa na kung’atwa na mdudu na hutibu vizuri  na haraka!

Kwa mapishi matamu ya pasta na grainZidisha utamu na ladha kwa kutumia tea bags pembeni mwa sufuria unayopikia pasta ,quinoa,wali,au aina yoyote ya nafaka.Manjano iliyosagwa ni tamu kwenye wali,Rooibos ni tamu ikichanganywa na oatmeal,na jasmine green tea ikichangnywa na yenye ladha kwenye pasta!

Huzuia kutu kwa sufuriaTannis husaidia oxidation,ambayo unaweza kutumia kuondoa kutu! Tumia kwa kufuta kutu kwenye pots,sufuria,na vifaa mbalimbali jikoni na utensils kwa kutumia tea bags kabla ya kuacha kukauka kwenye shelves.

Huzuia wadudu

Wadudu majumbani kama vile inzi na panya hawapendi harufu ya chai.Acha tea bags chache zikauke baada ya matumizi, weka ndani ya makabati.Aina ya mint ni nzuri kwa hili,na tea bags zilizotumika italeta athari zaidi ya harufu nzuri ndani ya kabati na itaua vijidudu.

Rutubisha mbolea yakoKunyunyizia kilichokuwemo kwenye tea bags iliyotumika kwenye mbolea itaongeza mchakato wa kuozesha zaidi,itasaidia mabaki ya chakula kuoza haraka.Ongeza majani ya chai katika mbolea yako husaidia kuzalisha bacteria ambao watazalisha rutuba sana kwa mimea yako,na hutengeneza mbolea kuwa ni yenye rutuba unapoongezea kwenye bustani yako au mimea nyumbani kwako.

kupambana na mafuta

Ukali wa chai wa hali ya juu pia hufanya kazi nzuri  kwa kuondoa mafuta .Tumia tea bags chache tia kwenye dishwasher pindi uoshapo  sufuria na bakuli zenye mgando wa mafuta,na tumia tea bags kama facial cleanser!


Share and enjoy!










Friday, April 8, 2022

Mahitaji ya Msingi ya Mapambo ya Kila Chumba Katika Nyumba Yako

10:17 PM // by Kalma // No comments

Mahitaji ya Msingi ya Mapambo ya Kila Chumba Katika Nyumba Yako

Unaweza kuwa na mtindo wa mapambo ya jumla uliochaguliwa kwa nyumba yako yote, lakini kwa mtindo wa jumla, kila chumba kina kusudio na mtindo wake. Jinsi matumizi ya chumba,kinatumiwa  na nani, inapaswa kuzingatiwa unapopanga kila chumba na kuchagua vifaa,mapambo, na uzuri na aina ya mapambo hayo.Zingatia mahitaji ya kila chumba na muhusika binafsi, na mapambo kulingana na nafasi ya hicho chumba. Mapambo ya nyumba yanapaswa kuonyesha hisia na ladha yenye maslahi binafsi, lakini lazima pia izingatie kazi maalum  ya hivyo vyumba.

Living rooms(sebule ya kupumzika na familia)

Sebule

Sebule zinaweza kutumika kwa  kazi nyingi, ni chumba rasmi kinatumika kwa kusalimiana na wageni,ni sehemu hata familia inatumia kusoma kwa Pamoja, ni sehemu ya burudani,kufurahia na kucheka Pamoja,na kucheza pia.Kwa nyumba za kisasa, sebule ni chumba kikubwa kimekuwa karibu na kuhusishwa Pamoja na jiko na dining area.Kubwa la kuzingatia ni kuchagua haswa mahala kwa ajili ya sebule au living room na haswa kuweka eneoau sehemu ya mazungumzo. Chaguo lako na mipangilio ya hiyo sebule yapaswa kiuzingatia akilini mwako.Hapo ndipo unaweza kusonga na mipangilio jinsi ya pa kuweka taa,sehemu ya zulia au rugs,marembo ya sanaa na mengineyo.

Vyumba vya kulala(Bedrooms)

Unatumia theluthi moja ya maisha yako kwenye chumba cha kulala, kwa hivyo unapaswa kuzingatia kwa uangalifu mikakati ya kupafanya mahali pazuri. Anza na kuchagua kitanda na fanicha zingine za chumba cha kulala. Wakati unaweza kuokoa pesa katika maeneo mengine,nunua godoro na mito bora na huo ndio  uwekezaji mzuri.Chaguo lako la rangi pia ni muhimu kwenye chumba cha kulala-chagua rangi zisizokolea ikiwa wewe ni mtu wa asubuhi, au rangi zilizokolea kama wewe ni wa kuchelewa. Taa ya chumba cha kulala ni muhimu kwa kuweka mood au hali nzuri, na piaIkiwa huna sehemu kubwa,tafuta ideas ya kupamba chumba kidogo kipendeze.Na vyumba vya kulala vya wageni vina mahitaji yao ya kipekee kwenye  kupamba.

Vyumba vya watotoKwa mapambo ya vyumba vya watoto, bado ni mazoea ya kawaida kutumia mandhari ambayo kwa ajili ya  wavulana na wasichana, ingawa wazazi wa kileo wameazidisha kutengeneza kufanya vyumba vya watoto kuwa vya kijinsia zaidi.Chumba cha mtoto mchanga kina mahitaji yake ya kupamba, haswa ambapo familia za vijana ambazo bajeti inaweza kuzingatiwa.

Bafu ya kisasaJe! Unataka kubadilisha bafu lako kuwa spa ya kifahari? Angalia ideas za bafu , pamoja kukifanya chumba kihisi ni mapumziko  na cha kisasa, na jinsi ya kuchagua makabati, tile, sinki, vioo, taa, na marembo. Katika bafu dogo, changamoto ni kuliremba ili lionekane kubwa.Ikiwa bafuni yako mpya inajumuisha mradi kamili wa kurekebisha, tafuta vidokezo juu ya kufanya liwe zuri na la kisasa. Maamuzi mengine muhimu yatakuwa kuchagua rangi na kuchagua sink zuri na marembo ya kuvutia.

JikoniJikoni kunaweza kuwa ni chumba cha gharama kubwa kurekebisha, kwa hivyo unatakiwa kupanga kwa uangalifu mradi  huo wako. Ikiwa urekebishaji kamili haitoshelezi na budget yako,basi tumia njia rahisi kuleta muonekano,ikiwemo usafi wa kina yaani deep cleaning,kurudia rangi,kuweka taa za kisasa,kubadili makabati,kuongeza mapambo,kubadilisha sink,mifereji na mabomba.Mwishowe, chaguo mapambo pekee na rahisi yanayoweza kufanya jiko lionekane jipya kabisa.Na kwa kweli,kwa  uchaguzi huu wa mapambo ni sehemu kuu ya  uboreshaji wowote wa jikoni ya bajeti  ndogo ya mradi huo.

Chumba cha kulia(Dining Rooms)Meza katika chumba cha kula  yaani dining room table ni kitu muhimu humo,kwa hivyo chaguo na uwekaji wake ni muhimu katika mapambo. Kuchagua fanicha sahihi inaweza kuwa muhimu sana kwa chumba kidogo cha kula. Vitu vingine muhimu vya kuzingatia ni viti na taa za kuning’inia au  chandelier — ambazo zote husaidia kufafanua mtindo wako na kuweka sauti ya chakula. Mwishowe, zingatia kwenye mapazia na vitambaa vya kutandika mezani na marembo mengine.

Foyers

Foyer inapaswa kuwa nafasi ya kukaribishia ambayo huweka muonekano wa  eneo la kupumzika, lakini pia kuna mambo mengi ya kuzingatiwa unapobuni na kupamba foyer yako. Sakafu, vifaa vya kuhifadhia, na aina ya marembo ni mambo muhimu katika kubuni foyer.

 Ofisi ya NyumbaniUtakuwa na mahitaji tofauti ikiwa utaona wateja katika ofisi yako ya nyumbani na kutumia nafasi hiyo kwa sababu za kitaalam. Lakini hata ikiwa ni mahali tu kwako kwa ajili ya ,kufanya biashara ya na familia, kuna vidokezo maalum vya kupanga na kupamba ofisi ya nyumbani. Pale ambapo bajeti inazingatiwa, tafuta chaguzi za kuokoa pesa.


SHARE AND ENJOY !