• LinkedIn
  • Join Us on Google Plus!
  • Subcribe to Our RSS Feed

Wednesday, November 29, 2017

Kusafisha microwave

4:12 AM // by Kalma // No comments

Kusafisha microwave

Mnato wa chakula kwenye microwave unaonekana vibaya,harufu sio nzuri,na hupunguza thamani ya microwave jikoni.Kwa bahati,microwave ni rahisi kusafisha ukijua.

Vinegar

        Glass inayofaa kwa microwave au bakuli yenye nusu maji changanya na 1 kijiko cha kula cha white vinegar.Tia ndani ya microwave.
Washa kwa dakika 5.Utahitaji dakika chache kwa microwave zenye nguvu zaidi,wakati ukisubiria hapo hapo kwa mara ya kwanza.Njia hii itayeyusha ukuta wa microwave na kugandua vilivyogandia.
Toa kama ni glass au bakuli,tumia kitambaa safi kwa kufutia au paper towel.Ondoa sahani ile ya kioo osha kama chombo kawaida,tumia dishwasher kama una muda.

Ndimu au Limao


   Kata ndimu au limao nusu.Tia maji nusu kijiko cha kula kwenye bakuli na vipande vya ndimu.Washa kwa dakika moja au ndimu imekua ya moto na uchafu umeganduka.Tumia kitambaa safi kufutia.Osha sahani kama kawaida.
Kwasababu ndimu imechemka husafisha vizuri kiasili kwa kibebeo (dustbin)cha taka za jikoni zikate vipande vidogo dogo zaidi na osha na maji mengi.  

Sabuni ya vyombo


Chukua bakuli tia maji ya moto ,tia sabuni ya vyombo kwa kiasi unachohitaji.Washa microwave kwa dakika moja mpaka uchafu uyeyuke.Tumia kitambaa au sponji safi kwa kufuta.Unaweza tumia baking soda ina harufu nzuri.

    Window Cleaner


  Changanya maji na window cleaner kwa maji ya uvuguvugu.Mchanganyiko huu utasafisha ndani na nje ya microwave.
    Futa ndani  kwa kuloweka sponji au kitambaa ndani ya mchanganyiko huo,toa sahani ya microwave safisha ndani na nje hadi uchafu uishe.Hakikisha microwave haijawashwa pindi usafishapo.

Loweka madoa kwa window cleaner kwa dakika 5 kabla ya kusugua.Suuza kitambaa au sponji kwa maji safi na ufute na window cleaner, kwa sababu ni dawa na sio nzuri kwa chakula.Rudia mpaka uhakikishe imeisha na microwave safi. 
      

       Kama baadhi ya madoa hayajatoka tumia kitambaa lowanisha na Olive Oil safisha tena.
Kuwa muangalifu na dawa au sabuni aina nyingine utumiazo kusafishia microwave.Kwa mfano,usitumie dodoki lililolowekwa ndani ya microwave inaweza kushika nyaya zilizolegea ikasababisha hatari. Kutumia dawa zisizo salama ni hatari .Pendelea vitu vya asili kama vinegar,ndimu n.k

Acha microwave ikauke.Hakikisha harufu nzuri ya microwave.Kama bado ina harufu ya window cleaner chukua kitambaa safi kisuuze na maji safi futia tena kwa mara nyingine.

Safisha nje ya microwave.Window cleaner ni salama kutumia kwenye milango ya microwave,vitasa,viwashio,na pembe zake.Futa vizuri mpaka vitakate. 

Tuesday, November 21, 2017

Jinsi ya kung’arisha tiles

2:36 AM // by Kalma // No comments

Jinsi ya kung’arisha tiles

Achana na kufagia na kudeki kila siku vipi unaweza kung’arisha tiles zilizofubaa,tiles zisizo ng’aa tena?Usikate tamaa,kuna njia ya kurudisha mng’ao kwa tiles zako tena.Njia hizi tumejaribu na zikafaa na kuleta mng’ao kwa tiles.
Vinegar na maji ya uvuguvugu
Tuanze na hii lakini inafanya kazi vizuri sana.Hii njia ni common imezoeleka sana hata pindi usafishapo kila mara.Vinegar hung’arisha vizuri na huondoa madoa mpaka tiles za ukutani sehemu ya kupikia.Kumbuka usitumie vinegar kwenye sakafu ya mbao ni asidi ambayo itaharibu hilo eneo.Suuza eneo hilo kwa maji ya baridi baada ya kusugua tumia vinegar.

Furniture Polish
Hii ni nyepesi lakini nzuri nayo kung’arishia tiles zako.Unachotakiwa kupulizia kwenye kitambaa cha kusafishia au kitambaa cha tea towel kwa mipulizo kumi(10) ya furniture polish.Weka kitambaa kwa sakafu yako na utumie mgongo wa brush kupolish kwenye tiles zako.Angalia vizuri uliposugua patakua panateleza kwa saa chache mpaka patakavyokuka.
Mswaki na dawa ya meno



Naamini watu wengi wanawaza jinsi ya tiles zao kung’ara.Njia moja tuliyoigundua kutumika iko mikononi mwako.Tumia mswaki chakavu na dawa ya meno,tumia kusugua tilea na kuondoa uchafu.Ukimaliza utasafisha uchafu uliomwagika kwenye mikono.Ni usumbufu?Tunahisi hivyo.
Dekio la kuaminika

Hii iko pale pale lakini ni kifaa  muhimu.Wataalamu baadhi wanasema maji ni kiungo muhimu kwa kusafishia tiles.Kwa hiyo,ni jinsi gani unatumia dekio lako kuleta mng’ao kwa tiles zako.Kama hilo dekio linatumika kila mahala basi hakikisha unalisafisha kwa maji ya moto kabla ya kusafishia tiles zako.Safisha vizuri ndoo ya kudekia tiles zako,weka nusu maji moto utumie kusafishia likiwa safi .
  Baking Soda
Je cooker lako au jiko la umeme linachafua tiles za ukutani jikoni kwako?Muda mwingi hautaona, lakini bakteria wanajenga humo kama hautakua makini na hilo.Njia ya kusafisha kuu kwa tiles zilong’ang’ania mafuta ni mchanganyiko wa baking soda na maji ya vuguvugu.Chukua bakuli kubwa lenye maji ya uvuguvugu ,na vijiko vya kula kadhaa vya baking soda tumia kwa kusugua tiles hizo.
Maji ya ndimu

Njia hii imezoeleka sana kwa matumizi mbalimbali majumbani inaweza kutumika kama aina ya kusafishia na kinywaji kwa upande mwingine.Kamua ndimu kwenye kitambaa,sugua kwenye tiles chafu na suuza kwa maji ya uvuguvugu.Baada ya kutumia chochote chenye asidi  futa eneo hilo na kitambaa safi laini.
Tiles zina sifa ya kusafishika haraka na zina asili ya kujilinda na layer za uchafu kwahiyo usiwe na wasiwasi wa kubadilisha kila mwaka.

Tips hizo juu ni rahisi na zitakusaidia kuleta mng’ao!

Sunday, November 19, 2017

Ondoa stress wakati wa kuhama

6:12 AM // by Kalma // 1 comment

Ondoa stress wakati wa kuhama 
Kuhama ni wasiwasi ulojaa msongo wa mawazo (stressful).


Ni kipindi cha hisia zaidi ambacho ni kigumu kukusanya au kupack kila kitu ndani ya nyumba ulipoishi.


Na zaidi kuondoa maisha ya vitu bila kuvichanganya,ni rahisi kuelewa kuwa ni balaa.Pamoja na mipango midogo tu na muono wa mbali,ni ngumu kuhama bila ya stress.Hizi ni step rahisi ukizifuatilia zitakurahisishia kuhama kwako

Jipe muda wa kutosha
Kuhama peke yake ni shughuli pevu.Na mwanzo wa kufungasha hautakufanya usiwe na haraka ya kumaliza,na huleta hamasa ya kuvipakua kiukweli.


Ukijipa muda wa kutosha utapanga vitu vizuri,hautavitupia au kurundika vitu kwenye maboksi.Muda wa kutosha wa kupanga,kuweka sawa,na kusafisha utashangaa hautakusababishia stress kabisaa.

Tengeneza orodha(Checklist)

Hakikisha vitu vyako havipotei kipindi hiki.Kuhamisha vitu vya thamani viwe kwa mpangilio.

Weka orodha ya vitu unavyotaka vipangwe na iwe rahisi kwako kuifuatisha orodha yako.Njia hii itakurahisishia kutosahau hata funguo au bakuli ndogo  ndogo zile.
Panga mizigo vizuri
Kwa kawaida inaonekana kupanga mizigo ndani ya vifungashio chochote ndo suluhu kwa kuepuka usumbufu.Hii inaweza kuleta shida mbele ya safari yako.

Fikiria utakavyorundika mizigo ya maboksi ndani ya truck utakalosafirishia mizigo na uharibifu wa baadhi ya vitu vitatumia muda wako mwingi,na mizigo mingine hata kuanguka.Badala yake,unaweza kukodi wahamishaji mizigo au nunua maboksi na upange mizigo vizuri.

Na maboksi madogo madogo yatasaidia kutorundika mizigo mingi ambayo husababisha maboksi kuchanika au kutobolewa wakati wa kuhamisha.Maboksi ya size ndogo yatakurahisishia kuhifadhi mizigo kwa salama zaidi.

Safisha pindi unavyopanga

Hakuna kigumu kama kila kitu kitakua kwenye boksi,kikubwa unachotakiwa ni muda mwingi utatumia kuchunguza vurugu zilizobakia.Ondoa wasiwasi kwa kusafisha unapoondoka.
Kufungasha vya jikoni?


Toa uchafu kwenye kabati za jikoni na countertops kwa kusafisha.
Umetia mizigo ya bafuni kwenye maboksi?Safisha kidogo bathtub wakati wa kupanga vifaa vya bafuni au chooni,futa pawe safi ukimaliza.

Kusafisha wakati unahama,pindi mizigo yote umeshaipaki  kitachobakia kikubwa ni kufagia au kudeki,huondoa wasiwasi kwa vitu vidogo dogo.

Label, Label, Label!


Kupata muda wa kupanga vizuri ni vizuri sana tena sana,lakini bila ya kulebo vizuri,mizigo ambayo itabaki utaipanga vizuri nayo.Kuhakikisha kila boksi la mzigo liko tayari kwa kuhamishwa au kupakizwa kwenye chombo cha usafiri kuelekea inapokwenda,na huzuia kuvurugika na kuhangaika kutafuta miswaki ilipo,ni muhimu kulebo boksi za mizigo.

Taarifa ya ziada ya mzigo hurahisisha kazi ya kupangua na kupanga upya.Tunasahauri  alama za rangi kwa vyumba kurahisisha,Kuona kwa uhakiki wa mizigo iliyofungashwa.Hakikisha unabandika vizuri lebo zako kwenye maboksi ili zisije kutoka na kupotea!

Ziada ya kulabel vyumba, ambavyo ni

Wakati unapanga nyumba au ofisi yako itapokua,nafasi kubwa ya usaidizi ni kulebo maeneo hata wanaokusaidia kupanga huwa ni kazi rahisi kujua huu mzigo ni wa chumba kwa mfano cha watoto n.k.

Hupunguza mkanganyiko wa maboksi kama la jikoni kwenda chumbani,kwahiyo lebo  ya milango ya nyumba unayohamia.


Tumia rangi ile ile uliotumia kulebo maboksi ya mizigo kurahisisha kazi kuwa laini kwa kiwango cha juu!