• LinkedIn
  • Join Us on Google Plus!
  • Subcribe to Our RSS Feed

Wednesday, June 10, 2015

Faida ya salad

6:46 AM // by Kalma // No comments

Faida ya salad
Kutumia au kula salad kila siku huleta faida nyingi mwilini. Hata hivyo salad ni afya na lishe rahisi ambayo mtu anatakiwa iwe ni tabia ajizoeshe nayo katika mlo wake.
Ni rahisi kuitengeneza,salad hukuweka karibu kila siku kwa kupata mboga mboga na matunda kama ilivoshauriwa.Unaweza kuongeza mafuta iwapo utakua unakula kila siku matunda na mboga mboga  na bado ukajenga afya yako  kutokea faida za salads.
 Fiber
Faida kuu ya salad ni kupatikana kwa fiber.Kula salad hutengeneza fiber nyingi mwilini,ambayo hupambana na vimbizi au shibe na inapunguza cholesterol.Fiber ipatikanayo kwenye salad husaidia kushiba haraka na kula kidogo.
Hii husaidia kupunguza uzito kwa baadhi  wasiopenda.Sababu salad ni shibe tosha,kula kabla hujala chakula kikuu(main meal)hupunguza kiasi cha calories ambacho ungeongezea tokea mlo wako.Kiasi kidogo cha calories unachokula kutokana na fiber  hupunguza uzito.
M-badala unaofaa
Wasomi wameonyesha  watu wengi  hawali  vyakula vya lishe na afya kama vilivoshauriwa.Wanapendekeza zaidi kula salad na matunda zaidi.Kula salad na matunda kila siku ni m-badala unaofaa  kwa mboga mboga na matunda,ambayo yanasababisha lishe na afya nyingi inayotakiwa mwilini.

Antioxidants
Mara kwa mara ukila salad ya kijani au green salad,unapata  kiasi kikubwa cha juu cha damu  yenye nguvu ya antioxidants.Mboga ina antioxidants muhimu sana kama vitamin C, lycopene, beta carotene na folic acid inalinda na madhara ya miale ya jua. Antioxidants ina sifa  ya kulinda dalili za uzee.
 Mafuta
Kwa kula salad,utakua umeongeza kuipata fat vizuri.Na mafuta hayo hupatikana kwa parachichi,karanga,au olive oil katika salad yako.Husaidia mwili kufyonza phytochemicals vizuri inayotakiwa mwilini.
  
Salads ina hasara kidogo au haina hasara kabisa, ambayo ni maandalizi yake na hutumia muda.

Saturday, June 6, 2015

5 Matunda kwa afya na mng’ao wa ngozi

4:05 AM // by Kalma // No comments

5 Matunda kwa afya na mng’ao wa ngozi
Kupatikana kwa 5 mazuri matunda fresh kwa afya na mng’ao wa ngozi hupendeza na kuvutia kwa kila mmoja wetu.Ni vizuri kuyapata katika kila mlo wako wa kila siku.!”Maisha ya kawaida hutofautiana kwa kuyapata matunda haya kwa kila mlo wako wa kila siku ambayo utang’aza ngozi yako na kuimarisha afya yako.Matunda husaidia kusafisha uchafu wa mwilini,kutengeneza na kurembesha ngozi,hydration ya kiasili,muonekano na mnga’ao wa ngozi,hutengeneza ngozi kuwa na muoekano wa ujana kila siku,na kutengeneza ngozi nyororo na laini. 
Matunda ni salama bila ya madhara yoyote kwa upande wowote wa kiafya ya mwili kwa muda wote.
Hayana sumu na yenye manufaa mengi katika kuboresha lishe na afya nzuri ya mwili na ngozi wa ujumla.
Ndizi
Ndizi ina wingi wa  Vitamini kama A, B na E. Hufanya kazi ya anti-ageing. Chagua tunda hili kwa kusafishia uso(facial)tumia ndizi iliosagwa changanya na asali kwa kung’arisha ngozi.Ni chanzo kikuu cha fibre ,madini,magnesium,na potassium,husaidia kurahisisha mzunguko wa damu mwilini na kujenga vilinda mwili imara.Ni tunda zuri kwa m-badala wa kurudisha afya kama kiburudisho katika mlo wako. 
 Papai
Ina antioxidants na enzyme waitwao Papain, papai hulinda na uchafu kwenye ngozi na huondoa seli mfu zinazotumika kwenye ngozi.Pakaa uso taratibu kwa dakika kadhaa,husafisha na hulainisha ngozi yako.Saga papai changanya na vijiko 2 vya chakula vya asali au maziwa ya mtindi,tumia mchanganyiko huo kama mask.Tumia maji ya uvuguvugu kwa kunawia baada ya dakika 20 kisha pakaa moisturizer utaona tofauti.
 Ndimu
Ndimu ina Vitamin C nyingi na hutumika kama bleach ambayo ni cleanser nzuri  huondoa mikunjo,makovu na madoa doa,na kupauka kwa ngozi.Anza siku yako kwa kunywa maji ya uvuguvugu yaliyochanganywa na kijiko cha ndimu na kijiko cha chai cha asali ukiwa hujala kitu.Mchanganyiko huu husaidia kupambana na cellulite na kusafisha ngozi yako kwa ndani zaidi.Kinywaji hiki hupunguza na kuondoa mikunjo kwenye ngozi na husababisha mng’ao asilia.

Chungwa
Machungwa yana Vitamin C,kwahiyo huongeza mng’ao wa ngozi.Huondoa mikunjo na hupunguza kuzeeka kwa ngozi.Kausha maganda ya machungwa yasage kisha yahifadhi kwa container zuri.Tumia kwa kupakaa kama scrub mara moja au mbili kwa wiki kwa kusafishia uso na kung’arisha ngozi. 
Apple
Tunda hili  yana antioxidant, hulinda kuharibika kwa seli na tishu na yanafanya kazi ya kulinda uzee kwa ngozi.Hupunguza mikunjo na kusafisha mistari inayojitokeza kwenye ngozi na kusafisha ngozi pia.Tengeneza juice ya apple changanya na asali pakaa usoni,ikikauka utaosha.Ni mask nzuri yenye kusafisha na kulainisha ngozi na kuifanya ngozi yako ing’ae na kuvutia.





Wednesday, May 27, 2015

VYAKULA VINAVYOBORESHA KUMBUKUMBU

7:25 AM // by Kalma // No comments

Ni jambo zuri kujua aina ya vyakula vinathamani zipi katika miili yetu.Chakula ni jinsi tunavyokitumia sisi wenyewe ,na bora zaidi kukiangalia faida ya chakula,kama ni chanzo cha nguvu mwilini mwetu.Tukiwa na ufahamu wa faida za chakula itatusaidia kula vyakula vizuri zaidi katika ubora wa afya,kwa kujisikia tuko vizuri,kiafya na kiakili pia.Nilikua naangalia njia za kukuza na kuboresha kumbukumbu,nilichogundua ni kwamba vyakula tunavyokula ni chanzo kikuu cha hili.La msingi tule vyakula vyenye kuujenga mwili vizuri.
 Chai(tea)
Faida ya chai huonekana kama ina mwisho-lakini huathiri kumbukumbu chai imehusika.Antioxidants inayopatikana kwenye chai ina  polyphenols –huboresha kumbukumbu,na hufanya kazi ya utambuzi katika akili.Chai ya kijani na nyeusi inazuia kazi ya enzymes wawili (acetylcholinesterase na butyrylcholinesterase), ambao wanashabihiana na ukuaji na maendeleo ya vijidudu vya Alzheimer.Kama unataka kuboresha kumbukumbu tumia sana chai,na ni vizuri ya kutengeneza mwenyewe,unaweza kuweka viungo vya asili unavovipenda na chai yako ikawa tamu ladha yake.




Rosemary
Kisomi zaidi ilionekana hata harufu tu ya rosemaru huboresha kumbukumbu ya muda mrefu na mfupi pia,na hata mahesabu ya kiakili,kutokea na compounds zinazopatikana kwenye harufu yake.Unaweza ukapanda nyumbani kwako ukawa unaipata harufu hiyo au kwenye chakula kwa kutumia mimea inapatikana kwenye olive oil.


 Kiazi sukari(beets)
Vyakula vyenye Nitrate nyingi kimojawapo ni kiazi sukari,huongeza msukumo wa damu,hufanya akili yako kuwa nyepesi na sharp na hulinda na matatizo ya akili.

 Mbegu za alizeti
Karanga na mbegu inasambaza mwilini omega-3 fatty acids,ambayo ni maarufu kwa kuboresha akili.Mbegu kama za alizeti ina chanzo kizuri cha vitamin E, husaidia kulinda seli za mishipa ya akili isiathiriwe.Kula karanga na mbegu hujenga afya na mwili pia.

Vyakula vyote ni vizuri kupata katika mlo wako wa kila siku.Uwezo wa kuboresha akili ni sehemu ndogo ya ujumla ya faida za kiafya mwilini.Tuweke mikakati ya kuangalia chakula tunavyokula na familia zetu kiwe ni njia mojawapo nay a muhimu katika kujenga afya,kutia nguvu,na tuwe wenye furaha katika maisha yetu ya kila siku. 


 cake yenye mbegu za alizeti.
 mbegu za alizeti zilorostiwa.


SHARE !

Friday, May 22, 2015

VIUNGO NA FAIDA ZAKE

10:06 AM // by Kalma // No comments

VIUNGO, 
Ni mpenzi wa viungo sana,na jiko langu limerembwa na aina tofauti tofauti  pia ya viungo.Zinavutia rangi zake,na vyenye mvuto wa asili harufu yake yenye kuleta hamu ya kula.
Visiwani haswa Zanzibar, Tanga siwezi kuiacha Morrocco hutumia sana viungo,Sio tu kuongeza ladha ya chakula bali pia vina faida nyingi za kiafya na urembo pia.Ni kitu kizuri kujifunza vipi viungo vitatusaidia katika maisha yetu ya kila siku. 
Viungo maarufu vinatumika sana,na Morrocco zaidi katika upishi wao ni: 



Chumvi,pilipili,tangawizi,manjano,(turmeric),pilipili mbuzi(paprika),jira au binzari nyembembe au uzile(cumin),zafarani(saffron) .
Hizo chache hapo juu huenda zikatusaidia katika afya zetu….
Tangawizi  
Njano isokooza rangi yake na harufu kali,inasifika kuwa ni kiungo kizuri chenye  faida nyingi kiafya.Kama unahisi uchovu,au tumbo limevurugika,tangawizi husaidia kutoa hayo udhia.Kuanzia mmeng’enyo chakula mbaya au uliokuwa slow,kutibu joints pia,tafuna kipande kidogo au weka kwenye kinywaji cha moto italeta nafuu.

Manjano (Turmeric)
Hiki ni kiungo kimojawapo kinatumika sana kipindi cha baridi kali huleta ujoto na harufu yake nzuri.Manjano ni yenye asili ya anti-inflamatory hutumika sana kwenye dawa za ayurvedic.Husaidia kuboost immune system,na pindi usikiapo baridi kali mwilini.Na hutumika kupakaa usoni na ni kujisugulia mwilini,hutoa uchafu,hufanya ngozi kuwa laini na hung’risha rangi ya ngozi kuwa yenye mvuto.huleta rangi kwenye chakula.




Pilipili mbuzi au boga(Paprika)
Hii ina lishe nyingi za kiafya katika mwili wetu,na sana Vitamin A.Kijiko cha chai kimoja cha rangi nyekundu ina zaidi ya 100%  ya mahitaji ya kiafya mwilini ya kila siku.Kama vitamin A  husaidia kuona,huongeza madini ya chuma ambayo hutia nguvu mifupa.
 supu yenye paprika.
  Jira (Cumin)
Jira ina nguvu sana,huwa ni kama badala ya chumvi.Ina kiasi cha Sodium kidogo,tumia zaidi hii badala ya chumvi husaidia kushusha blood pressure,ni yenye ladha nzuri katika chakula.Jira ni chanzo kizuri cha Vitamin B,ambayo inasaidia kuleta usingizi.Jaribu kula ndizi iliyochanganywa na jira kabla ya kwenda kitandani kama una shida ya kupata usingizi. 



Zaafarani(Saffron)
Japokuwa hiki kiungo ni cha gharama ,ni kizuri kwa chenye afya nyingi nyingi.Husaidia digestion na inflammation,unaweza ukatumia zaafarani kwa njia nyingi na kuweka kwenye chakula pia.Tengeneza mask ya  maziwa ya zaafarani,chukua zaafarani weka kwenye maziwa mabichi ambayo hayajachemshwa.Kisha iache zaafarani kwa saa mbili kabla ya kuyatumia,maziwa yatakuwa rangi nyekundu.kisha pakaa usoni,iache kwa dakika kumi10 kabla ya kuosha uso.Kiungo hiki husaidia kusafisha uso na ngozi iliokauka na huondoa madoa! 
 Cake ya strwabery na zaafarani.