• LinkedIn
  • Join Us on Google Plus!
  • Subcribe to Our RSS Feed

Wednesday, January 22, 2014

NJIA 10 KUU ZA KUTIBU FANGASI YA KUCHA.

6:09 AM // by Kalma // No comments

KUTIBU FANGASI YA KUCHA

Fangasi ya kucha,hujulikana kama onychomycosis ni tatizo sugu linalowakumba wanawake hata wanaume pia.Dalili zake inflammation,kuvimba,maumivu ya hali ya juu,kucha kusinyaa au kuwasha Visababishi vingine ya fangasi ya kucha ni kuvaa synthetic socks,kuwa katika mazingira ya  unyevu nyevu,PH level ya ngozi kuwa sio kawaida,mfumo wa immune system mdogo,viatu vyenye majasho,uchafu,na kisukari.
Kama fangasi ya kucha haitachukuliwa tahadhari mara kwa mara huweza kusababisha kukatika kwa kucha,splitting,na hata kuimaliza kucha na kutoka kabisa.well,habari nzuri ni kwamba fangasi ya kucha hutibika bila hata ya kutumia pesa kwa bill za dawa.Kuna njia za kufanya zinatibu fangasi kwa mwezi au miezi miwili.
Njia kuu 10 za kutibu fangasi ya kucha.
1.Tea tree oil
Tea tree oil ina antiseptic kama zilokuwemo kwenye fungicide ambayo husaidia sana katika kutibu aina hii ya fangasi.Haya mafuta hutumika kutibu athari katika ngozi pia.Kama unatatizo la aina hii ya fangasi ,chukua tea tree oil yenyewe tumia pamba pangusia mafuta hayo katika sehemu ilo athirika acha kwa dakika 10 kisha mswaki kwa kusugulia kwenye hiyo sehemu yenye fangasi.Kabla ya kupakaa mafuta hayo kwenye ngozi,yachanganye na olive oil sawa na kiasi cha tea tree oil au tumia thyme oil.Hutibu fangasi kama sio ya muda mrefu au iliokomaa,au sugu.
  
 
2.Baking soda
Baking soda ni rahisi kupatikana nyumbani hutibu fangasi pia.Chukua kikombe nusu cha baking soda,vikombe vinne vya maji moto,moja ya nne ¼ ya kikombe cha peroxide na nusu kikombe cha chumvi ya Epsom.Changanya hizo zote  vizuri na kisha moja ya nne ¼ ya kikombe cha white vinegar katika mchanganyiko huo.Lowesha sehemu ilioathirika na vinegar kwa dakika chache kisha pakaa ule mchanganyiko kwenye hiyo sehemu tumia pamba na kisha ifunge hiyo pamba kwenye hiyo sehemu iloathirika kwa fangasi.Tumia njia hii kila baada ya saa 10 kwa muda wa wiki nne. 
3.Mafuta ya machungwa
Njia nyingine ni kutumia mafuta ya machungwa.Aina zote za machungwa ni antifungal nayo huweza kutibu fungasi.Kwa kudondoshea kitone cha mafuta hayo kila siku katika hapo penye fangasi,juu,chini na katikati ya kucha na iache kwa saa moja.Pia unaweza ukaichanganya hayo mafuta ya machungwa sawa na mafuta mengine yoyote ,kama mafuta ya mbegu za zabibu.Kama mafuta ya machungwa yataleta allergy na kusababisha madhara,ni vizuri kujaribisha kwenye ngozi kwanza kabla ya kuyatumia kwa kujitibu

4.White vinegar
White vinegar ni moja wapo ya tiba nzuri ya fangasi ya kucha.Changanya kama kijiko kimoja cha vinegar na vijiko viwili vya maji ya vuguvugu.Kisha lowesha sehemu iloathirika na mchanganyiko huo kwa dakika kumi hadi kumi na tano kila siku.Kama utahisi ngozi inaungua zidisha maji kidogo kwa vinegar.Ni muhimu kukausha eneo la fangasi baada ya kunawa au kuoga,la sivyo fangasi itaenea na kuambukiza kwengine.

5.Kitunguu thoum
Kitunguu thoum kina allicin,ambayo ina antifungal na hutibu fangasi pia.Kwa kutibu mara ya kwanza tumia mafuta ya kitunguu thoum changanya sawa na vinegar namaanisha kipimo cha vinegar na mafuta viwe sawa.kisha pakaa eneo la fangasi na pembeni zake kisha funga tumia bandage.Ikiwa mafuta ya thoum hayapatikani,tengeneza mwenyewe kwa kuisaga,chukua vitunguu thoum viwili kisha changanya na vijiko viwili vya kula vya olive oil.kisha iache kwa saa  24.Hata kula kitunguu thoum kimoja kila siku nayo ni dawa ya fangasi pia.

6.Juisi ya siki ya apple
Juisi ya siki ya apple ina acid ya asili na huweza kulinda na fangasi ya kucha kuendelea.hapo hapo juisi hii hupambana na vijidudu na huua bacteria.Chukua juisi ya siki ya apple changanya sawa kwa sawa na maji kwa kipimo chochote utachotumia.Kisha utaitumia kwa kuloweshea sehemu ya fangasi kila siku kwa muda wa nusu saa.Kama utafanya hivi kwa muda wa wiki kadhaa utaona mabadiliko kwa muda mfupi tu.Njia nyingine unga wa ground rice changanya na vijiko vichache vya juisi ya siki ya apple,pakaa na husaidia kuondoa ngozi iliokufa na kuiweka ngozi yako kuwa laini.


7. Listerine Mouth Wash
Listerine mouth wash inaua bacteria na germs mdomoni huweza kutibu fangasi ya kucha pia.Hii ni kwa sababu mouth wash hii ina alcohol yenye nguvu nyingi za antiseptic huweza kupambana na bacteria na fangasi pia.Chukua pamba lowesha hii mouth wash na vinegar na maji ya ndimu ambayo hayajachanganywa na maji.Kisha unaweza loweka miguu au mguu au ukapakaa mchanganyiko huo kwa dakika kumi hadi kumi na tano kila siku na kisha tumia kwa kusugulia pia.Fanya hivyo kila siku mpaka ile kucha ya zamani itaondoka itakuja mpya na nzuri.


8. Lavender Oil
Lavender oil ina volatile na antiseptic properties ambayo ina uwezo wa kupambana na aina yoyote ya infection na kuilinda ngozi kuharibika pia.Chukua kiasi cha lavender oil na tea tree oil changanya vizuri kisha fanya kuipasha iwe ya uvuguvugu kidogo.Kisha funga kwa kutumia pamba katika kidole mara mbili au tatu kwa siku.Na vizuri pia kupakaa mchanganyiko huo kabla ya kulala.

9. Oregano Oil
Oregano oil ina antiseptic, antibacterial, anti-parasitical, antiviral, analgesic na antifungal pia.Huweza tumika kutibu fangasi ya kucha.Chukua matone mawili ya mafuta ya oregano na changanya na vijiko viwili vya chai vya olive oil.kisha pakaa kwa fangasi kwa siku mara moja.Fanya hivyo kwa muda wa wiki tatu. 
 
10.Juisi ya ndimu
Juisi ya ndimu ina antiseptic na ni antifungal pia.Citric acid iliyomo kwenye ndimu husaidia kumaliza fangasi za kucha na kutoambukiza.Chukua juisi fresh ya ndimu na pakaa direct sehemu yenye fangasi na uache kwa dakika 10 kabla ya kusuuza na maji ya uvuguvugu.Tiba hii irudiwe kila siku kwa muda wa mwezi mmoja mpaka uone matokeo mazuri.Njia nyingine changanya juisi ya ndimu sawasawa na olive oil na tumia mchanganyiko huo kusugulia au massage sehemu yenye fangasi.Olive oil itafanya ngozi yako kuwa laini na juisi ya ndimu itasaidia kuzuia madhara ya fangasi.
Kwa hizo tiba za asili hapo juu za kutibu fangasi ya kucha,matokeo yake hutegemeana na juhudi ya kuzitumia hizo dawa.Itumike kwa muda wa kuanzia mwezi na kuendelea ndipo utapoona matokeo mazuri. 


SHARE AND ENJOY !



0 comments:

Post a Comment