• LinkedIn
  • Join Us on Google Plus!
  • Subcribe to Our RSS Feed

Monday, December 9, 2013

TIBA YA ASILI YA MAUMIVU YA KICHWA.

8:38 AM // by Kalma // 2 comments

Maumivu ya kichwa sio fun.Wakati wowote huweza kukutokea,huwezi jua…sidhani kama unaweza kufanya kitu.Kwa upande wangu mimi ikinitokea huwa natamani kufanya lolote maumivu yapotee na yasirudie tena ikiwezekana.Kipindi cha kubadili hali ya hewa ,kichwa huwa ni kawaida kila mtu kuumia au kuumwa,na haswaa kukiwa baridi sana,naziweka hizi tukifanya hivi tunaweza punguza maumivu ya kichwa,kwa kutumia tiba asili.
Dawa nazo sio nzuri kwa afya zetu wote.
Kuna aina nyingi na tofauti za maumivu ya kichwa,na tofauti ya hisia za mwili na tiba zake, najaribu kutoa aina tofauti ya tiba za asili ambazo huenda ikawepo moja wapo kuwa tiba kwako wewe na mimi kadhalika.
1. Maji
Dehydration inajulikana sababu mojawapo kuu ya maumivu ya kichwa.Tunajua kwamba tunahitajika kunywa maji ya kutosha kwa siku,kiasi cha glasi nane(8),la kushanagaza ni rahisi kusema kuliko kutekeleza.Kama unahisi maumivu ya kichwa yanakuanza,la kwanza jiulize umekunywa maji kiasi gani kwa siku hiyo?na kisha kunywa maji .Kama kinga awali,ni vizuri kunywa maji ya kutosha kila siku.Utapata faida nyingi nyengine  ndani yake,maji huondoa sumu toka mwilini hupitia kwenye ngozi,hiyo ni faida mojawapo, zipo nyingi tu.
2. Chai
Kunywa chai kwa wingi-yenye Tangawizi,kivumbazi(peppermint), au chamomile –husaidia kutuliza maumivu ya kichwa ya aina zote .Tangawizi ni nzuri kwa  migraines huzuia  synthesis ya prostaglandin (ambayo husaidia kutuma dalili za maumivu kwenye ubongo),na kulainisha au kutuliza kujisikia uchovu,ambao uchovu huendana na migraines au kipanda uso.
Kivumbazi(peppermint) husaidia kupunguza na kutuliza maumivu pia-na tokapo kivumbazi(peppermint) nayo huondoa uchovu wa mwili,nayo pia hutibu kipanda uso. Chomomile hutumika  kutibu na kukinga maumivu ya kichwa,hupumzisha misuli na husaidia kupunguza stress (chanzo kikuu cha kuumwa ni kichwa).
3. Essential Oil
Aromatherapy ilianza tumika karne kama kituliza maumivu .Ni aina moja wapo matata ya kutuliza maumivu ya kichwa nayo ni lavender(mvinyo), peppermint,(kivumbazi) na eucalyptus. Matumizi yake,changanya mafuta na maji au mafuta ya nazi na sugua temples,shingo,na mabegani.Njia nyingine kutumia aromatherapy ni kuongezea tone ya mafuta ya maji katika maji ya uvuguvugu ya kuogea.Mchanganyiko huo wa maji ya uvuguvugu na mafuta yenye harufu kama karafuu,mafuta ya nazi, huwa ni kituliza maumivu na hukufanya ujisikie umeuondoa uchovu na kuondoa maumivu ya kichwa.  
4. Acupressure
Acupressure husaidia kutuliza maumivu kwa kutumia kulainisha mishipa ilojikaza au kukakamaa  na kuondoa  endorphins,ni dawa asili ya mwili.
Na sehemu nzuri za acupressure kwa maumivu ya kichwa ni:  
- paji la uso(komwe)  — kwenye kope
- temples
- nyuma shingoni — sehemu ya katikati
- juu ya kichwa(kichwani) — upande wa katikati, mstari kwa kuelekea masikioni
- mikono —ukuta kati ya kidole gumba na kidole shahada  
- juu ya mguu — katikati ya kidole gumba na kidole kinachofuatia
Tumia kidole gumba kupakaa au kufanya massage hiyo sehemu kwa mtindo wa  kuzunguka.Endelea kufanya hivyo kwa 1-2dakika,au mpaka utapojisikia kunaanza kuwa pamoto.

 Tahadhari : Acupressure hii huweza sababisha kizunguzungu au  lightheadedness,chukua tahadhari kabla haijatokea hivi.
5. Mapumziko
Kupumzika ni sababu yatosha  kujisikia vizuri wakati wote-na maumivu ya kichwa yakiwemo kwenye list.maumivu haya sana husababishwa na stress na wasiwasi,tafuta namna ya kujipumzisha husaidia kutibu shida hii muda huo huo,na huzuia kutorudia maumivu ya kichwa kabisa.
6. Apple Cider Vinegar
Tiba hii ni mapendekezo ya mdau wangu mmoja hivi.(nakushukuru sana!!) japo research ilifanyika  na ikaonekana ni tiba ya kichwa.Kuna aina mbili za kufanya: njia ya ingestion na  vaporization(uvukizi). Njia ya ingest,unaweza changanya vijiko 2 vya kula vya apple cider vinegar katika glasi ya maji na kunywa yote kwa pamoja.hii inafanya damu kutembea vizuri katika mwili,na vile vile husaidia kubalansisha kiasi cha PH mwilini.
Njia ya vapor unachukua vijiko 2 vya kula vya apple cider vinegar katika sufuria na vikombe 2 vya  maji yaliyochujwa kisha chemsha.Ukianza kuona mvuke sasa zima jiko.
chukua taulo weka kichwani mwako kisha inamia huo mvuke wa huo mchanganyiko,hema kidogo dogo  mpaka utapoona maumivu yanapungua au kuisha kabisa.


SHARE AND ENJOY !

2 comments:

  1. apple cider vinegar ni juisi ya siki ya apple. Kwa hiyo hayo maneno mekundu ndio unahitaji tafsiri yake

    ReplyDelete