• LinkedIn
  • Join Us on Google Plus!
  • Subcribe to Our RSS Feed

Monday, October 4, 2021

10 Makosa ya kupanga sebule(living Room)

1:09 AM // by Kalma // No comments

10 Makosa ya kupanga sebule(living Room)

Sebuleni ni mahala ambapo watu watakujua au kukujadili ulivyo kimsingi hutakiwi kufanya makosa unapoiremba yaani designing.
Haya ni makosa ya kawaida ambayo yatachukiza sebule yako,unatakiwa uyaepuke!
Sebule ni moyo wa nyumba ambayo inaleta mvuto wa kwanza.Ni kiwakilishi ambacho sio cha moja kwa moja kinachokuwakilisha tabia na muonekano wa uhalisisa wako. Imezoeleka,pindi tunavyoremba sebuleni ,tunafikiria zaidi kwa vile tunavyovipenda na hamu na hutuangalii kiundani makosa tunayoweza kuyafanya pindi tunapoiremba.

Umuhimu wa kuangalia sebule ni pale marembo yanaendana na hali halisi ya sebule na muonekano wa hicho chumba.Kumkodi mtaaalam wa kazi hizo sio kwa ajili ya matendo,na hata hivyo ni ghali.Ni nyumba yako na wewe mwenyewe unatakiwa uwe m bunifu wa upambaji kutokana na nafasi ya sebule yako.

Hizi njia nzuri za kupamba sebule yako kama utajua makosa ya kawaida katika upambaji,tumia unachokijua katika upambaji na ilete tija.

Hii inaweza kuwa chochote cha muonekano muhimu kwa upambaji wako.Kosa kuu na muhimu sebuleni ni vurugu katika upangaji,ambao huonyesha kabisa kumepangwa bila mpangilio.Haijalishi ni nyumba mpya au imerekebishwa,kuwa makini na makosa haya ya kikawaida sana yanayofanyika katika kupamba sebule zetu.Mabadiliko madogo machache yanaleta muonekano wa mvuto tofauti.

Taa(Lighting)
Kama hazikuwekwa vizuri,itachukiza chumba chako.Hakikisha kuna taa kila upande.Kuwa na taa za juu peke yake nalo ni kosa pia.Tumia mwanga wa LED zilizofichwa kwenye siling ni wazo zuri .

Wrong Carpet 
Kila mara hakikisha carpet unazotumia zinaendana na size na shepu ya chumba .Kuwa makini wakati wa kuchagua rangi pia.
Mpangilio(Positioning) 


Hakikisha ya kuwa furniture zote ziko sehemu sahihi.Kuweka TV sehemu isiyo sahihi ni kosa lilozoeleka sana haswa katika kupamba sebule.

Sofa kukaa ukutani 

Kuweka sofa ukutani ni kosa la uharibifu.Kama unadhani itafanya sebule kuvutia,sio kweli ,unaiharibu sebule yako 
Rangi za giza ukutani(Dark Wall Colour)


Kupakaa rangi za giza yaani dark hufanya chumba kuonekana kidogo na mrundikano.Kama unapenda rangi za kukolea sana,tumia ukuta wa eneo moja kung’arisha,na tumia rangi za mwangaza kwa pande nyingine za ukuta.
Mpango wa kizamani
Japokuwa wanasema "old is gold",haibebi ukweli katika fashion za kizamani kwenye furniture.Kwahiyo,weka furniture zinazoendana na wakati za kisasa kupendezesha sebule yako.

Kupuuza sehemu muhimu katika chumba
Baada ya yote,sebule ni sehemu ya kualika wageni na ni sehemu ya kupumzika wewe mwenyewe baada ya mchoko na mihangaiko.Usipafanye ni sehemu ya kukaa kula,kunywa,kulala,kufanyia kazi,mazoezi,au kuweka meza yako ya ofisini.
Mapambo madogo dogo

 Kuzidisha sana mapambo sebuleni sio ndio kutavutia hii sio kweli.Kuipamba sebule kwa mapambo ya kisanii yaani art gallery nayo ni makosa yaliyozoeleka kwa watu wengi.Weka furniture chache na zipange sehemu nzuri ziendeane na chumba.
Pazia
Urefu wa pazia dirishani ni fashion ya kizamani (Window-length curtains).Tumia urefu wa pazia tokea sakafuni na magongo ya pazia nzuri halafu yawe marefu. 
Hii huleta muonekano mzuri sebuleni.


Share! Comments! Like ! 
Be hygienic and Smart !














































 

0 comments:

Post a Comment