• LinkedIn
  • Join Us on Google Plus!
  • Subcribe to Our RSS Feed

Thursday, November 11, 2021

KUONDOA M-BA.

1:24 AM // by Kalma // No comments

KUONDOA M-BA

M-ba(dandruff)huenda ikawa ni madhara ya ngozi kavu,au hali ya ngozi inayoitwa seborrheic dermatitis.Huweza sababishwa na eczema, psoriasis, au, kawaida zaidi,kasi ya kukua kwa fungasi anaitwa malassezia. Dawa za kutibu inaweza kuwa shampoo pamoja na zinc pyrithione, ambayo hukomesha fangasi na bacteria, ketoconazole, nayo inapambana na fangasi; coal tar na selenium sulfide,ambayo hukuza na kuua seli zilokufa katika ngozi ya kichwa; na salicylic acid, hii hulainisha flakes ambayo huondoka kwa kuoshwa.
Tumia hizi njia za asili.
Aspirin
Aspirin inafanya kazi ya (salicylic acid) kama shampoo nyingi za dawa.Chukua vidonge viwili vya asprin visage viwe unga kabisa, weka kwenye shampoo unayotumia osha nywele siku zote.Pakaa kwenye nywele kwa dakika 1-2,suuza nywele ,osha na shampoo iso na asprin.


Tea tree oil
Imegundulika kuwa shampoo zenye asilimia 5% ya mafuta ya tea tree hupunguza makali ya m-ba.Weka matone machache kwenye shampoo yako pindi unapoosha nywele.


Baking soda
Jiko lako ni ufunguo wa kutengeneza mambo mazuri,kuanzia mapishi, afya na urembo pia. Lowanisha nywele zako kisha sugua baking soda ya ujazo wa kiganja chako.Usitumie shampoo kisha zioshe.Baking soda huondoa au kupunguza fangasi ambao sababu ya m-ba.Nywele zako zinaweza zikawa kavuu mwanzoni,lakini baada ya wiki kadhaa ngozi ya kichwa itaanza kutoa mafuta ya asili,na zikafanya nywele zako kuwa nzuri na kuepusha ukoko.


Apple cider vinegar
Dr. Mehmet Oz swears juu ya  apple cider vinegar kama ni tiba ya m-ba,kama ilivyo acidity ya vinegar  ya apple hubadilisha pH ya ngozi yako, kuifanya kuwa ngumu kwa bacteria kuzaliana.Changanya robo kikombe cha vinegar ya apple na robo kikombe cha maji katika chupa ya pulizo(spray bottle) na kisha pulizia kwenye ngozi ya kichwa chako.Funika kichwa na taulo na kaa kwa dakika 15 mpaka saa nzima,osha nywele kama kawaida.Fanya hivi mara mbili kwa wiki.

Mouthwash
Kutibu m-ba waliokomaa kichwani,osha nywele kwa shampoo yako unayotumia,kisha suuza na mouthwash.Kisha tumia conditioner.Mouthwash  ni anti-fungal husaidia kulinda na m-ba ambao wanasababisha hata bacteria kukua.


Mafuta ya nazi
Crunchybetty.com amesema  coconut oil is a "tried and true" na ni tiba ya m-ba,na hunukia vizuri pia.Kabla ya kuoga,sugua 3-5 vijiko vya chai vya mafuta ya nazi katika ngozi yako na uache kwa saa nzima.Osha na shampoo kawaida.Unaweza kutumia shampoo zenye mafuta ya nazi pia.


Ndimu
M-ba hauwezi kudumu kama friji lako.Vijiko 2 vya chai vya maji ya ndimu sugua kwenye ngozi ya kichwani na osha na maji.Kisha koroga kijiko 1 cha chai ya maji ya ndimu ndani ya kikombe cha maji kisha suuza nywele kwa mchanganyiko huo.Fanya hivyo kila siku mpaka m-ba wapotee kabisa.Asidi iliyoko kwenye ndimu husaidia kubalansi pH ya ngozi yako,ambayo husaidia kuondoa m-ba pia. 


Chumvi
Chumvi nayo ni nzuri na huondoa m-ba kabla ya shampoo.Chukua saltshaker kisha nyunyizia chumvi kwenye ngozi ya kichwani.kisha sugua nywele na ngozi.Utahisi ukavu na nywele zimenywea hapo itakua tayari kuoshwa na shampoo.


Aloe vera
Usisugue aloe vera katika ngozi ya nywele kabla ya shampoo.Madhara ya kupoa kwa aloe vera husababisha kuwashwa na maumivu.




Kitunguu thoum
Kitunguu thoum ni anti-fungal huondoa vizuri na kwa haraka m-ba wanaosababisha bacteria. Saga kitunguu thoum kisha sugua kwenye ngozi ya kichwa.Kuepukana na harufu,unashauriwa uchanganye kitunguu thoum na asali na sugua kwenye ngozi kabla ya kuosha kama kawaida.

Olive oil
Kwa usiku mzima lowanisha nywele na mafuta ya olive.Sugua kwenye  ngozi ya nywele matone kumi ya mafuta kisha vaa kofia usiku kucha.Osha na shampoo yako asubuhi.Kwa tiba ya haraka,tumia shampoo ambayo ina olive oil. 




0 comments:

Post a Comment