• LinkedIn
  • Join Us on Google Plus!
  • Subcribe to Our RSS Feed

Wednesday, April 12, 2017

Kupanga dressing table

5:27 AM // by Kalma // No comments

Kupanga dressing table
Dressing table inavurugika sana kwa sababu ni mahala pakuhifadhia vitu vidogo dogo vingi,kama vipodozi,dawa,vipambio,urembo wa dhahabu,silver n.k.Hata hivyo,dressing table bado inatakiwa iwe safi mara zote na imepangika vizuri ili iwe rahisi kupata vitu pindi utumiapo
 Tips:
Toa au tupa vipodozi vyote visivyotumika.
Hii husababisha dressing table kuwa imejaa na vurugu.Unafikiri kuwa manukato au perfumes,lotions,na vichupa mbali mbali huonekana vizuri .Achilia mbali mawazo hayo,usifikiri hivyo.Unatakiwa utupe vyote visivyotumika kuleta muonekano mzuri na wa kuvutia kwa dressing table yako.Na vile vile utapata nafasi ya kutosha kwa ajili ya vingine muhimu na vipya.
 
Panga kulingana na aina
Jingine,panga vitu kwa makundi kwenye dressing table.Tofautisha mapambo,dawa,mkoba wa huduma ya kwanza,na urembo.Weka powder ya usoni,foundation, lipstick, mascara, eyebrow pencil,na vipambio vingine kundi lake kwasababu hutumika wakati.Kwa hiyo,unatakiwa uwe na mkebe wa kubebea vipodozi kuhifadhi humo.Hata dhahabu,silver na mapambo ya vito na mengineyo yakae kwenye mkebe wake.Hapo utaweka lotion, night cream, sunblock,na vingine vinavyofanana na hivi.Kingine,utazipanga perfume kwa usafi mzuri.Kama una aina ya manukato tofauti tofauti kwa mfano ya usiku na mchana nayo utayawekea kwa makundi yake halikadhalika udi n.k.





Kumbukumbu za upangaji
Kitu gani unatumia sana kwa dressing table yako?Utasema ni vya kujipambia,mashanuo na vitana,lotions, perfumes,na jeweleries. Hta dawa hutumika pale unaposikia maumivu.Hifadhi kwenye droo vile visivyotumika mara kwa mara na weka sehemu ya karibu vile vinavyotumika kila mara ili kuvipata kwa urahisi.




Pendelea kupanga dressing table mara tu inapovurugika .

Tutumie dressing table yako tushare pamoja!

0 comments:

Post a Comment