• LinkedIn
  • Join Us on Google Plus!
  • Subcribe to Our RSS Feed

Wednesday, April 5, 2017

Kusafisha Oven haijawahi kusafishwa(na ukafanikiwa)

4:07 AM // by Kalma // No comments

Kusafisha Oven haijawahi kusafishwa(na ukafanikiwa)

Hii iko serious hivi muda huu 10:30 usiku oven lako limerowekwa na baking soda,racks za oven zimelowekwa kwa bathtub,birika la chai (buli) linatokota maji moto kwa kusafishia juu ya oven,na mumeo kapiga magoti hahaha…nimecheka apo!anasafisha sakafu kwa sponji kwa sababu unagundua muda umeenda na huna dekio au tambara la usafi (mop).(kiukweli ningemwambia aache!)

Tunaita  usafi wa kina(deep cleaning),
Sakamia ikianza hii,hairudi nyuma.
Tukifanya usafi tunapendelea njia za kisasa zaidi kuboresha kazi yetu.Sakamia hatu
tumii madawa makali sana,tumejifunza ni Baking soda kwa kusafishia oven.
Koroga uji wa baking soda na maji pakaa kwenye oven yako.Iache kwa usiku mzima.Unasafisha uji ulioganda kwa kupangusa na maji.Halafu,pulizia vinegar kumalizia uchafu wa baking soda. Futa vizuri.
Muhimu: 
Ufunguo muhimu wa kuitumia baking soda,pindi unaposafisha oven,unapaswa kuipa muda ili ifanye kazi.Kusubiri kwa saa 12 au usiku mzima ndio tiketi yake.
Asubuhi yake unasugua ndani tumia sponji,halafu futa kwa kitambaa safi laini.Muda huo unapulizia vinegar kwa kitambaa unachopangusia mpaka uchafu wa baking soda uishe wote.Utaona rangi ya kijivu na brown yote imeondoka ,na sehemu zote zikibaki safi na mng’ao wa kuvutia.
Mlango wa oven
Baada ya kuloweka na baking soda,nakusugua kutoa uchafu,hapa unaangalia kama oven yako inatoka kioo utatoa utasafisha  hakikisha pameng’aa.
Racks:
Zinafurahia kulowekwa kwa beseni la kuogea(bath tub)!sio lazima beseni najua utaniuliza la kwangu lipo chumbani inakuaje?unaloweka kwa sabuni ya kuoshea vyombo.
Muhimu:
 kama umeamua kusafishia kwenye beseni hakikisha unaweka kitambaa wakati unaziloweka la sivyo zitachubua bathtub.
Tumia sabuni kwa kuzisugua vizuri hadi ziwe kama mpya.
Juu ya jiko (Stovetop):
Tumia maji ya uvuguvugu kuloweka zile chuma za kupikia kukata mafuta.Tia sabuni kali acha kwa 15-20 dakika,kabla ya kusugua.
Unaweza tumia dishwasher(mashine ya kuoshea vyombo)lakini bado haitakatishi sana.Niambie mdau wangu we ni njia gani hutumia zikang’aa?Utendelea kusugua na kufuta kwa kitambaa kisafi laini.
Mwishowe,ni sakafu yaani floor :
Ni safi! Mshukuru aliyekusaidia mumeo,msaidizi n.k amesugua kwa sponji,hao ni wale wakupendao.
Una ratiba gani ya usafi wa kina kwako?
   Sakamia Cleaners
Be hygienic and smart!!

0 comments:

Post a Comment