• LinkedIn
  • Join Us on Google Plus!
  • Subcribe to Our RSS Feed

Tuesday, November 26, 2013

JINSI YA KUSAFISHA LAPTOP.

7:08 AM // by Kalma // 1 comment

JINSI YA KUSAFISHA LAPTOP

Hivi lini ilikuwa mwisho wa kusafisha laptop yako? je keys za laptop yako zimeanza kugoma?laptop yako mpya imeanza kuonekana kama ya zamani?
Kwa kukaa tu kwenye desk laptop yako huwa chafu,sikwambii zinazozunguka katika siti za magari.Vumbi hujikusanya ndani ya laptop na sana sana kwenye feni.Huilazimisha feni kuzunguka zaidi ambayo hatari yake ni kuiruhusu kupata moto husababisha hata kufa .
Ni vizuri kuishi maisha ya raha na yenye afya na yakipendezeshwa na laptop yako safiii…
Fuatilia njia hizi huenda ikatatua huo uchafu wa laptop yako.
Tafuta dawa ya kusafishia-kwenye screen au kioo inabidi utumie “screen cleaner”.Kwa sehemu 
nyingine  chukua  bakuli tia sabuni kiasi,na Isopropyl alcohol.


Changanya mchanganyiko huo.
Kisha tumia
Chupa zile za kupulizia dawa ambazo zina mfuniko wa kupulizia.
Zima compyuta yako na toa betri-usisafishe wakati unatumia.
Toa mouse,disc,cd’s,Usb,waya na chochote kilichochomekwa.
Chukua ile dawa pulizia,kuondoa uchafu.

Kama uchafu uko mwingi unaweza chukua kisu ukatoa keys kwa uangalifu,waeza haribu connector, au kuumia wewe mwenye .
Weka bakuli la maji na sabuni kidogo,tia vile vikasha vya keys ndani ya maji hayo kwa muda kubanduka yale mauchafu yalogandia.Ukisugua tumia mkono au mswaki au brush ndogo ,tumia mswaki ambao hautumiki.
Tia bakuli nyingine maji ya uvguvugu na nusu kipimo cha Isopropyl alcohol.loweka kitambaa kidogo kwenye huo mchanganyiko ,kamua maji yasichuruzikie kwenye laptop.tumia kufutia ndani ya keyboards na uso wa laptop sio screen,ieleweke hapoo.

Safisha katika mikunjo ya laptop tumia ule mchanganyiko wa kupulizia mpaka isafishike vizuri.
Iache laptop kwenye hewa ipate kukauka.Usifunge mfuniko wa laptop. Kama ulitoa keys tokea keyboards anza kuzifuta kwa  kitambaa kikavu.


Anza kurudishia keys kwenye keyboards ukiwa una uhakika mashine yako imekauka vizuri.
Tumia dawa maalum kupangusia screen.Pulizia kisha futa na kitambaa kikavu.Hii iwe hatua ya mwisho katika usafi wako sababu isipate uchafu tena,pindi usafishapo sehemu nyingine.
Usitumie sabuni za kawaida huweza haribu screen yako au kupunguza performance yake,na hata uzuri wa mng’ao wa screen yako.
TIPS
Weka chakula mbali na laptop yako.Osha mikono kabla ya kutumia laptop yako .Kama utatoa keys,hakikisha unajua kurudishia,Tumia keyboard nyingine kugelezea kurudishia keys au print copy yake ili upate picha kamili ya keyboard ya laptop yako.Fanya hivyo kila unapotaka safisha laptop yako.

Pata kinywaji ukipendacho baada ya usafi huo na furahia usafi huo kwani umekusaidia kupunguza stress na umeinjoy piaUsiache kutembelea blog yetu ndani ya mtandao kujifunza mengi na mazuri zaidi.

1 comment:

  1. safi!!
    naipenda sana blogu yako na habarizako.
    Ni blogu ya kipekee na habari za kipekee.
    Hongera sana

    ReplyDelete