• LinkedIn
  • Join Us on Google Plus!
  • Subcribe to Our RSS Feed

Tuesday, November 26, 2013

KUONDOA CHUNUSI.

9:27 AM // by Kalma // 2 comments

CHUNUSI

Chunusi au Pimples ni aina ya doa au madoa yanayosababishwa na mafuta ya ziada yaliyokuwa trapped katika vinywelea.Nyingine ni Postules au Papules.Chunusi huweza tokea usoni,mabegani kifuani na hata mgongoni.
Chunusi  hutibika  kwa aina ya dawa za kuondoa makovu ambazo zimependekezwa na wataalamu,na hata kwa kununua za maduka ya dawa au urembo,kwa mtazamo wa kujitibu.

SABABISHI:
Ndani ya vinywelea kuna Sebaceous gland,ambayo inazalisha “Sebum”.Pindi layer ya nje ya ngozi inapoziba,seli ya ngozi zilokufa au kuisha, nyuma kushoto hufanya kuganda kama gundi na huganda na sebum.
Hii husababisha vinywelea kujifunga,na sana sana pindi pale ngozi inaposinyaa kama ya “kwapani”.Sebaceous glands huzalisha Sebum nyingi ambazo hujenga nyuma juu ya pale palipoziba,na hii  njia ya Sebum kuna kuwa na bacteria wakiwemo kama Propionibacterium acnes,husababisha madhara na kuungua ambayo huitwa chunusi.

TIBA ;
MADAWA YANAYOAGIZWA
Kuna cream kwa ajili ya kutibu chunusi.
Dawa ya kawaida inayotibu na inayojulikana kwa chunusi ni Benzoyl Peroxide na Salicylic Acid na antibacterial kama Triclosan,zote hizo ni aina ya dawa hupatikana kwa mfumo wa cream na gel na hutumika kwa kupakaa.Husaidia kutoa chunusi kwenye ngozi kwa haraka na hulainisha ngozi pia.Huondoa bacteria kwa haraka.Kabla ya kupakaa unatakiwa uoshe uso au sehemu husika kwa maji ya uvuguvugu na ukisha ukaushe na taulo safi.
Cleanser huweza tumika kuoshea kwa nia ya kupakaa dawa.
Rosecea hii sio kwa ajili ya madhara yatokanayo na bacteria.Madhara yalosababishwa na bacteria hutumika Tretinoin.

Kusafisha uso kuwa safi na kupakaa  cream yatosha kuwa tiba nzuri ya chunusi japo sio ya kudumu.
Aina ya kawaida na nzuri zaidi ni Benzoyl Peroxide,ina hatari ya ngozi kidogo huweza sababisha allergy.
Kwa sasa Nicotinamide hupakaliwa kwa kipindi imeonyesha kutibu zaidi kwa chunusi kuliko antibiotics kama Clindamycin.
Nicotinamide (VitaminB3)sio antibiotics na haina madhara pia.Ina faida ya kupunguza Hyperpigmentation ambayo  ni kisababishi cha chunusi.

DAWA(PRESCRIPTION  MEDICATION).
Dawa nyingine hulazimika kuandikiwa na watalam kwa tiba ya chunusi.Nayo ni Isotretinoin ambayo ni Retinoid.
Historia yake ni antibiotics kama Tetracyclin na Erthromycin zimetajwa.Nazo zilikuwa zinatibu zaidi kushinda Benzoyl Peroxide,Bacteria walikuwa sugu na ikashindwa kupambana nao .Na antibiotics zinaonekana zina madhara zaidi kuliko cream  mfano wa kuumiza tumbo,huweza kubadili rangi ya meno,zile antibiotics ziloelezwa na Dermatologist na wakashauri ni Doxycycline na Minocycline.Kwa ajili ya kuondoa  chunusi kwa mara moja.
Walishauri pia Accutane ambayo ilikuwa nzuri kwa kutibu chunusi nayo. Hii Accutane huweza sababisha madhara kama kutapika,kuharisha na matatizo ya uzazi kwa wanawake.

TIBA YA USAFI(HYGIENE).
Tumia njia hii mara kwa mara ;osha ngozi ilioathirika na chunusi,tumia natural cleanser,husaidia kupunguza seli za ngozi zilokufa na muingiliano wa bacteria ambazo ni sababu ya chunusi.
Japokuwa sio kama ndo inaweza kuondoa kabisa chunusi ila hupunguza kasi ya chunusi kuendelea na kuenea na hata kuzuia pia.
Chunusi ni ngumu kutoka na huchukua muda mrefu.Madawa yametengenezewa na madawa ambayo sio nzuuri kwa ngozi.Tumia njia hizi za asili zifuatazo;

CHUMVI(SEA SALT).
  • ·         Chumvi ina detoxifying qualities hufanya kazi nzuri ya kukausha na kuondoa chunusi na madoa pia.
  • ·         Chukua vijiko (3)vya chai vya chumvi weka ndani ya bakuli.
  • ·         1/2kikombe cha maji ya moto yalochemka sana,tia ndani ya bakuli uloweka chumvi.
  • ·         Changanya na koroga pamoja tumia kijiti cha cotton buds .
  • ·         Chukua upande wa kijiti hiko kina pamba kitakua kimelowa na maji yale .
  • ·         Kisha weka kwenye chunusi au doa na shilkilia  kwa dakika 10-20.
  • ·         Unaweza fanya mara mbili kwa siku mpaka chunusi zikauke.
  • ·         Unaweza tumia kitambaa kuwekea kwenye chunusi zilojikusanya sehemu moja nyingi.

BAKING SODA.
  • ·         Osha uso tumia cleanser au sabuni ya uso.
  • ·         Vijiko vya chai (8)vya baking soda weka kwenye chombo.
  • ·         Tia maji kwenye  chombo uloweka baking soda.
  • ·         Koroga vizuri,iwe laini na uji uji yani isiwe nyepesi wala nzito sana iwe creamy.
  • ·         Pakaa mchanganyiko huo katika chunusi .
  • ·         Subiri kwa dakika 15 mpaka ikauke.
  • ·         Osha na maji ya uvuguvugu.
  • ·         Fanya hivi kwa wiki mara mbili(2)mpaka chunusi zipotee au kukauka.
  • ·         Ikiwa uso utakuwa mkavu sana fanya mara moja(1)kwa wiki.ngozi ikianza kukauka zaidi  ni bora upate ushauri wa daktari. 
  •          Kumbuka kukauka kwa ngozi ni kawaida sababu chunusi husababishwa na mafuta yalozidi kwenye ngozi.

NJIA NYINGINE YA KUONDOA CHUNUSI NYUMBANI KWAKO.

Barafu(ice)
1.       Husaidia katika mzunguko wa damu katika sehemu iloathirika,huondoa uchafu na mafuta yalolundikana kwenye ngozi.
2.       Weka barafu kwenye kitambaa kisha weka sehemu ilo chunusi kwa dakika chache hivi kama unakanda.

Ndimu
1.       Ina Vitamin C,husaidia kukausha chunusi.
2.       Loweka kitambaa kwenye maji ya ndimu ilokamuliwa,kisha pakaa,fanya hivyo kabla ya kulala waeza osha asubuhi au kuosha baada ya nusu saa.Hakikisha unatumia ndimu ilo fresh ndio nzuri zaidi.


Asali
1.       Hii ina antibiotics na huzuia madhara ya bacteria,pakaa asali acha kwa nusu saa kisha osha na maji ya uvuguvugu .
2.       Fanya hivi mara mbili kwa siku.

Dawa ya meno
1.       Wakati unapiga mswaki asubuhi na jioni pakaa dawa hii pia kisha osha uso kwa maji ya uvuguvugu,na unaweza kulala nayo ukaosha asubuhi .
Steam
1.       Weka maji kwenye bakuli maji ya uvuguvugu kisha jifunuke na taulo kichwani ukiwa umeinamisha uso kwenye bakuli hili la maji kwa dakika 10-20.
Kitunguu thoum(garlic)
1.       Hii ni antifungal,antiviral,antiseptic,na ina sulfur pia.visage sugulia kwenye chunusi acha kwa dakika 5 kisha osha uso na maji ya uvguvugu .Hata kula inasaidia kupurify damu,ila usile sana ina madhara tumboni.

Peppermint
1.       Maji ya majani yake ukiweza yapata ,yasugulie au pakaa maji hayo kwa dakika (10).Osha uso kwa maji baridi.Hii ina antibacterial na antiviral.


Tango
1.       Ni antioxidant,ina Potassium,Vitamin A,C,n E.Loweka vipande vya tango kwenye maji kwa saa moja (1hr)virutubisho  kama VitaminA, Potassium na Chlorophyll vitaingia kwenye maji.Chuja maji na kunywa maji yake,au tumia kuoshea uso.

2.       Unaweza tumia kama mask.
3.       Saga tango moja kisha pakaa usoni kwa dakika(15)ikauke.kisha osha kwa maji ya uvuguvugu.

Papai
1.       Ni antioxidant,Vitamin A,hulainisha ngozi tumia kwa kupakaa kwenye chunusi.






2 comments:

  1. habari njema kwa sisi wenye chunusi.
    Rekebisha dawa ya "mswaki" isomeke dawa ya meno
    shukrani sana

    ReplyDelete