• LinkedIn
  • Join Us on Google Plus!
  • Subcribe to Our RSS Feed

Thursday, November 7, 2013

KULAINISHA VIGANJA .

12:32 AM // by Kalma // No comments

KULAINISHA VIGANJA

Moja ya hasara ya mwanamke aliye hodari na kazi za nyumbani ni viganja vya mikono kuwa vigumu au vikavu.Kama unafua na maji na sabuni,kuosha vyombo,kusafisha nyumba,kubadili watoto nepi au diapers,kupika  n.k . usishangae kuwa na viganja vigumu au vikavu.
        Hakuna haja ya kuogopa na toa wasiwasi hii ni aina ya kufanya mikono yako iwe laini na ya kuvutia.Huna haja ya kwenda kwa spa’s wala kwa wataalamu.Baada ya kazi zako fanya haya;
   Kunywa maji kwa wingi na  tumia njia hizi zifuatazo;

Chukua  container weka chumvi kiasi.
Weka olive oil ndani ya container.
Weka sabuni  ya maji ya kuoshea mikono,tumia aina unayoipenda inaweza kuwa anti-bacterial  au yoyote ya maji.Ni vizuri kutumia sabuni ya maji sababu hautaosheka vizuri mkono sababu maji na mafuta hayachanganyiki.
Kausha mikono yako vizuri,kisha weka mchanganyiko huo kwenye viganja vyako kisha sugua pole pole ,kiasi cha ½ kijiko cha chai.Sugua ndani na nje ya viganja na ndani ya vidole na kucha.
Osha kwa maji ya uvuguvugu .
Kausha mikono kwa kutumia taulo kavu.
Pakaa lotion ya mikono .
AU
Osha mikono na maji ya uvuguvugu na sabuni kuondoa grease na bacteria.kisha kausha na taulo kavu.

Chukua sukari  vijiko viwili(2) vya chai na  olive oil pia vijiko viwili(2).

Pakaa mikononi kwa pamoja haraka .
Sugua mikono yote kwa pamoja ndani na nje kwa kutumia  mchanganyiko huo.

Osha na maji ya uvuguvugu.

Tumia rose water pia nzuri .
Kisha pakaa lotion ya mkononi.

      Waweza tumia pia sunflower oil na hata mafuta ya nazi pia mazuri.

TIPS
Usifanye mara moja ukategemea matokeo ya kudumu au milele.Tumia baby oil au lotion kabla ya kulala.Tumia lotion zinazotengenezewa na mimea zaidi.Acha lotion kwa dakika kumi(10)kwenye viganja,ile layer ya juu ya ngozi itanyonya lotion na italoki moisture ndani ya ngozi.Fanya hivi mara mbili(2) kwa wiki.Vaa gloves au plastic wakati unafanya kazi kama kuosha vyombo au gardening.Tumia Vaseline.
Kwa mikono mikavu zaidi unaweza kulala na gloves ukiwa umepakaa lotion.

Usiache mikono kwenye maji baridi kwa muda mrefu,huondoa  mafuta na unyevu wa asili mikononi.
Kuwa muangalifu na aina ya lotion utayotumia kuepusha athari za allergies.
 Hizi ni aina ya lotion unaweza tumia kulainisha mikono : 
The body hemp hand protector, Aron moisture therapy intensive hand cream, L’Occitane shea Butter Hand Cream, Eurin Intensive Repair Extra Enriched Hand Crème, Ahava Source Mineral Hand Cream, Jaqua Raspberry Butter cream Frosting Hand Crème.


0 comments:

Post a Comment