• LinkedIn
  • Join Us on Google Plus!
  • Subcribe to Our RSS Feed

Wednesday, May 17, 2017

Jinsi ya kuondoa harufu mbaya kwa friji

1:36 AM // by Kalma // No comments

Jinsi ya kuondoa harufu mbaya kwa friji
 Kuweka friji kuwa fresh
Unukaji wa friji uko kinamna nyingi.Huweza sababishwa kwa kumagika kwa maziwa na hata mayai yaliyosahauliwa kwa muda mrefu.Ushawahi kusahau viazi katika kibebeo cha mboga mboga?Hua inaleta harufu mbaya kuliko unavyofikiria.Madoa mengine yanang’ang’ania kuliko mengine,madoa mengine ni ya asili,lakini sio wazo zuri kuyaacha kwasababu yanaweza kuenea na kuharibu kila sehemu ya friji na yakasababisha uharibifu hadi kwa miundo mbinu ikawa tabu kusafisha kwake.
Lakini subira ndogo tu na matunzo yanazaa mafanikio ya utunzaji wa friji lako.
Njia ni hizi zifuatazo:
Toa kila kitu nje
Hata kama umegundua sehemu yenye uchafu,unatakiwa utoe vitu vyote kwenye friji na friza.Kama una friji mbili unaweza hamishia vitu huko kwa muda.Kama uchafu ni sababu ya kuzima friji,usitoe vitu ukiwa hauko tayari kusafisha kwasababu friji linahifadhi kwa muda wa saa 4,kama itadumu imefungwa.
Osha kwa mkono bins na shelves





Toa shelves ,bins,droo,trei za barafu,na chochote kinachotoka na uvioshe kwenye sink tumia sabuni na maji moto.Kwa friji lenye harufu,changanya kijiko cha kula kimoja(1)cha chlorine bleach kwenye galoni la maji na tumia mchanganyiko huo kufutia kwenye shelfu chini na bins pia;suuza kwa maji safi na kausha kwa kitambaa safi.
Manukato ndani ya friji


Sasa utakua tayari kuosha ndani ya friji.Tumia mchanganyiko wa kikombe kimoja(1)cha baking soda kwa gallon la maji.Futa ndani ,chini kwa kutumia sponji ulowekee mchanganyiko huo.Kwa vifungashio vya chakula pitisha sponji juu kisha futa kwa kitambaa safi.Usitumie kifaa kigumu kwa kusugulia friji huweza kuchubua friji lako.
Kukausha

Hapa panataka subra kidogo.Kwa matokeo mazuri,unatakiwa uzime friji,acha milango wazi,uliache kwa siku nzima.Kama litaendelea kutoa harufu tumia mchanganyiko wa baking soda kufutia tena na uliache kwa siku nzima tena.Hapa kwa friji lenye harufu kali na haikufanikiwa kuisha .
Tip
kuileta harufu nzuri kwa friji,weka pamba ambazo zimelowekwa na vanilla ndani ya friji na friza halafu funga kwa saa kadhaa kabla ya kurudishia vitu.
Kusafisha evaporator
Kama bado kuna harufu na haijaisha,nafasi kubwa ya harufu itakua inatokea kwa evaporator coil,ambayo hutoa hewa ya baridi kwenye friji na friza.Coil,ikiambatana na feni husambaza hewa,zimewekwa ukutani  wa nyuma ya friji au friza.
Anza kwa kutoa screw ambazo zinashikilia kifungashio.Chomoa kwenye umeme na kitengeneza barafu. Toa na osha panel.Tumia chupa ya kipulizo yenye maji moto ya sabuni kwenye coil,zuia maji machafu yamwagikayo na kitambaa;rudia na maji safi kwa kusuuza.Iache coil ikauke kabisa kabla ya kuifunga na panel.
Kazi hii ni rahisi,hakikisha unaweka friji au friza sehemu ambayo unaweza kusafisha kwa nyuma.Tumia kitabu cha maelezo yaani manual kwa maelezo zaidi.
Jua kama una friji jipaya yaani ya kisasa yenye dual evaporator ,itakua ina coil mbili,moja ni kwa friza na nyingine kwa friji.Kama uchafu ni sehemu ya chakula yaani friji utasafisha coil husika.

0 comments:

Post a Comment