• LinkedIn
  • Join Us on Google Plus!
  • Subcribe to Our RSS Feed

Wednesday, May 3, 2017

Njia 5 za kutakatisha nguo nyeupe bila bleach

5:12 AM // by Kalma // No comments

Njia 5 za kutakatisha nguo nyeupe bila bleach
Achilia mbali kusugua kuondoa madoa,baking soda husaidia kutoa madoa na kuifanya nguo kuwa laini  yaani soft pindi ufuapo.Hakikisha unasuuza vizuri na sabuni utumiayo na punguza matumizi ya bleach kuanzia sasa.
Jinsi ya kutakatisha nguo nyeupe bila bleach
Nguo nyeupe hushika madoa kirahisi sana hata ukiwa makini,au hata baada ya kuvaliwa huanza kuleta rangi ya njano flani hivi. 
Kuifanya ing’ae siku zote kwa weupe wake, mara zote hutumika dawa zipatikanazo madukani kwa siku hizi,ambazo nyingi kati ya hayo madawa yana bleach na kuaminika ndio suluhisho bora zaidi kwa kung’arisha nguo nyeupe na nyinginezo.

Kiukweli hizi products zinafanya kazi vizuri yaani zinang’arisha vizuri,na huenda ikawa njia rahisi ya kupata mng’ao wa weupe katika nguo.Lakini madawa yaliyomo kwa dawa hizo sio nzuri kwa afya kabisa,ni hatarishi hata kwa mazingira yetu.
Kujilinda na vihatarishi kwa kutumia dawa za bleach na dawa zenye bleach,article ya leo tunataka kwa pamoja kushare njia za kufua na kung’arisha nguo zako kwenye  mazingira rafiki zaidi,kwa kutumia vitu asili ambavyo utavihifadhi  nyumbani kwako kutoa madoa na kung’arisha nguo zako na kurudisha weupe wake wa upya.
White vinegar
Potezea matumizi ya kutumia dawa za kuondoa madoa na uchafu sugu,white vinegar ni rahisi kuondoa madoa hayo na husaidia nguo kuwa soft kiasili badala ya kulainishwa na madawa mbalimbali.
  Tumia ½ -1 kikombe cha distilled white vinegar kufulia kawaida kila mara, na hata ndani ya washing mashine,na tumia mashine kawaida utumiavyo.
   Kama nguo zako zina madoa au uchafu shingoni,makwapani, mifukoni au sehemu yoyote,sugua kwa kutumia white vinegar maeneo hayo na iache kwa saa nzima kabla ya kufua .
Baking soda
Baking soda hii ni nyongeza ambayo inapatikana kirahisi,inapenya kwenye kina cha madoa katika nguo,huondoa madoa na kulainisha pia.
Weka ½ kikombe cha baking soda wakati wa kufua tumia kama dawa ya madoa na ufue kawaida. Kumbuka mara zote kutofautisha na usichanganye nguo nyeupe na za rangi. Kwa madoa sugu,changanya baking soda na maji ya ndimu kidogo moja kwa moja kwenye yale madoa.
Hydrogen peroxide
Hydrogen peroxide ni dawa nzuri sana kwa kuleta mng’ao kwa nguo nyeupe kwasababu haina bleach.
weka ½ kikombe cha 3% ya hydrogen peroxide pindi ufuapo.Tumia moja kwa moja kwenye madoa pia.
Maji ya ndimu
Maji ya ndimu nayo ni ya asili yanayotakatisha na kung’arisha kwenye kina cha fiber,huondoa madoa na uchafu na kuiacha nguo safi na manukato mazuri na nyeupe.
Tia maji kwa beseni na vipande vya ndimu,chemsha,kisha loweka nguo zako kwa muda wa saa nzima kabla ya kufua.
   Njia nyingine mchanganyiko wa maji na sabuni,kijiko cha chakula cha chumvi,na maji ya ndimu mbili.Loweka nguo kwa mchanganyiko huo,suuza na anika juani.
Maziwa
Hii hata sisi tumestaajabu,ni mshangao!unaweza tumia kung’arishia nguo zako na upya wa weupe kupatikana. Ushauri wa matumizi ni nguo za cotton haswaa na zile delicate fabrics.
Matumizi?
Tia nguo kwa beseni lenye maziwa na loweke kwa saa kadhaa,kabla ya kusuuza kawaida.
Tips
Nguo nyeupe inahitaji matunzo ya ziada ili iwe kwenye hali ya mng’ao na safi yenye rangi ya kuvutia.
Kama nguo nyeupe ndizo upendazo tuwe pamoja kwenye hizi tips:
    Epuka utumiaji wa bleach kwa nguo aina ya polyester au cotton-polyester, mchanganyiko wa  bleach na polyster unaweza kusababisha polyster  ikabadilika ikawa njano.
    Umakini zaidi kwa maji utumiayo pindi ufuapo,kama sio masafi husababisha nguo kuwa njano.
   Pindi ufuapo nguo nyeupe tia borax iliyochanganywa kwenye maji kulainisha nguo.Borax haileti madoa kwenye nguo.
    Jihadhari madoa doa kwenye nguo nyeupe,hakikisha hutumii perfume,deodorant,au kisababishi chochote cha madoa.Hizi ni sababu ya kufanya nguo kuwa njano.
    Mara zote anika nguo nyeupe juani,kwasababu UV rays husaidia kung’arisha zaidi.
SHARE AND ENJOY !

0 comments:

Post a Comment