• LinkedIn
  • Join Us on Google Plus!
  • Subcribe to Our RSS Feed

Saturday, May 6, 2017

Ng’arisha chumba chako

7:47 AM // by Kalma // No comments

Ng’arisha chumba chako
Kitanda, Furniture,mapambo,taa,pambo za ukutani & vioo   
       


 Unajua kwamba ni mapumziko tosha muonekano wa chumba chako kwa mabadiliko madogo tu?Huitaji furniture mpya  au kupaka rangi tena,japokuwa kupakaa rangi mpya nayo ni vizuri.Unaweza kubadili uonekano wa chumba chako kwa kukipangilia furniture hizo hizo ulizokuwa nazo,bila ya gharama yoyote.Kama hii haitoshi badili duvet cover,kwa kitanda chako au kitanda chako kihamishie upande mwingine.
Rangi za shuka

Kwa muda mrefu kidogo napendelea mashuka ya rangi zilizokooza ,familia yangu wanapenda pia tuliona tunaendeana . Kwa sasa nimebadili natumia rangi zilizopoa yaani cool colours au rangi za kizungu kwa jina lingine.Maua machache yenye rangi ya njano na zambarau,mito mingi mingi aina tofauti unachanganya rangi ya foronya.Hua najisikia mapumziko makuu niingiapo chumbani kwangu.
kioo
Hata ukiwa na chumba kidogo,unaweza kuongeza kioo upande mmoja wa kitandani  vile virefu designed kizuri kitu amaizing,utahisi chumba kikubwa kinawaka na kisafi.Vioo huvutia na kuongeza mwanga kwa chumba kidogo kinafaidi mwanga mwingi na ukubwa umeongezeka.
Maua
Maua yawe ya ukweli au ya mapambo hubadili muonekano wa chumba.Huongeza uhalisia na uzuri kila mahala.Unaliweka sehemu nzuri inayokupendeza basi huvutia kwa kuliangalia kwake na kuchanua kwake,huleta furaha litoapo harufu.Unalipamba vizuuri inaweza ikawa kwenye kona,au juu ya meza ndogo ya pembeni kitandani n.k.
Kiti 
kizuri chenye rangi nzuri inayoendana na mapambo ya ndani ya chumba .Utajishangaa saa zote upo chumbani kwako maana kinakupa faraja na kukupumzisha.Kiweke kwenye kona ambayo unaweza kusoma vitabu huku unaangalia dirisha,au upande iliko Tv,kama chumba cha ghorofa unaangalia view ya nje ukipata hali ya hewa fresh na salama kwa afya yako.
Yote hayo yatakupumzisha chumbani kwako kwa gharama nafuu .Najua unaweza kufanya vizuri zaidi .

ENJOY !


0 comments:

Post a Comment