• LinkedIn
  • Join Us on Google Plus!
  • Subcribe to Our RSS Feed

Thursday, August 5, 2021

4 Tips rahisi ya kupanga mashuka

1:54 AM // by Kalma // No comments

 4 Tips rahisi  ya kupanga mashuka

Sakamia cleaners imepanga nyumba kadhaa nguo pamoja na mashuka.Tukagundua njia rahisi ya kupanga kuleta mvuto na muonekano mzuri.Tips hizi zimesaidia zaidi kwa nguo za linen na nyinginezo. Na imezaa matunda makubwa mazuri ya kubadili muonekano wa kabati na mvuto pia.Na zaidi haswa kwenye mashuka 
Panga mashuka kwa size 

Nyumba nyingi zina aina tatu(3) au mbili za size ya vitanda na mashuka.Uliwahi kufikiria unaweza kuyasimamisha vizuri kwa bila mategemeo, ni ngumu kama utavyojaribu.Napendelea rangi nyeupe na cream na kuzipanga kwa size zake.Zipange sehemu ya wazi au kona kwa size na shepu yake kwa jinsi ulivyozikunja kuendeana na rangi zake,ni rahisi unapohitaji kutumia na kujua mpangilio wa mashuka hayo,na husave muda wa kutafuta na kuepusha kupangua.
Weka seti ya shuka ndani ya foronya
Inakurahisishia kuweka seti ya shuka na foronya zake zote ndani ya foronya moja.Zikunje kwa pamoja kwa mkunjo mzuri zikiwa safi hifadhi ndani ya foronya.Mazaga zaga yote ya seti ya shuka yatakua pamoja na safi .
Panga mashuka wima(vertically)
Tumezoea kuweka mashuka juu ya lingine.Ni njia nzuri lakini inasumbua wakati wa kutoa husababisha kuanguka na kuvurugika, haijalishi umeyapanga vizuri kiasi gani.Ni rahisi lakini inatumia muda mwingi mara kwa mara utawajibika kupanga.kwa kuyapanga wima huokoa muda na hayapanguki na rahisi kutoa unapohitaji kutumia.
Tenganisha kwa size na sehemu tofauti
Kujua size ya shuka na size za seti za shuka,panga kila size upande wake au shelf tofauti.Ni rahisi hata kwa familia kujua shuka ya size gani ipo sehemu gani bila ya kuvuruga.

Tunathubutu kukuambia kwa mpangilio wa tips hizi za mashuka umeletaa mvuto wa upangaji na usafi wa hali ya juu.Umesaidia kwa familia kujitegemea kwa kuchukua shuka bila kupangua na kuhakikisha ni safi pindi warudishapo.

  Tuambie ni njia gani unatumia kupanga mashuka yako yakaleta mvuto wa usafi?

0 comments:

Post a Comment