• LinkedIn
  • Join Us on Google Plus!
  • Subcribe to Our RSS Feed

Tuesday, October 29, 2013

KOME/MAKASHA (mussels or clams)

7:10 AM // by Kalma // No comments

KOME

Kome ni anajulikana kwa jina lingine kasha ni kitoweo kinopatikana kwa maji ya bahari au freshwater maji yaso chumvi.Ni kitoweo kwa matumizi ya familia na makazi ya watu wa pwani zaidi.
       Kome wanagamba wenyewe wako ndani.
Kome ni tofauti na chaza,wao ni wakubwa wakati chaza ni wadogo.
Chaza kwa kizungu ni Oyster na kome ni Mussels au clams.
      Neno "mussels"hutumika kumaanisha chakula kwa familia za mabaharia.
Kome wana gamba la rangi ya blue ilokooza,nyeusi,au brown,wenyewe wana rangi ya silver hivi .
    Freshwater ni kama Ziwa,Mto,vijito,maji ya mifereji.
Kome wanakula plankton na viumbe visivoonekana katika bahari ambao wanazama kwenye maji.
Wanapatikana milimani mwa maji.
        Wako jinsia ya kike na kiume.Fertilization yao hutokea nje ya mwili wao,huwa wana larvae kuanzia wiki tatu hadi sita.
       Kome hawa wanaliwa na binaadamu,samaki kama starfish,ndege wa baharini,na dogwhelk anapatikana baharini pia.
    Kome wa freshwater wanaliwa na Otters,raccons,ducks,na baboons wa Coast South Afrika na geese.
Sana sana hutumika kama chakula.
    Italy huchanganya na samaki wengine kwa chakula na wanapendelea wa kuchemsha na wanatia ndimu.
   Ufaransa wao hupatikana kwa jina la Eclade des moules wanawakausha na haswaa Biscay beach bay.
  Huweza kuliwa mchuzi kwa wali na supu pia
India hutumia kwa mkate kama tunda la mkate na mboga mboga pia.Na hutengeneza kwa nazi kama mchuzi kwa wali na viungo na pilipili.
         Kome anaweza kuchomwa,kukaangwa,berbeque,steam,kwa siagi au mafuta na mboga .
Wanatakiwa wawe hai kabla ya kupikwa.wana sumu ila huisha kwa kupikwa .na huchemshwa sana na kisha kumwagwa maji.
Hufunguka maganda wanavopikwa .Unaweza kuwapasua gamba na kuwatoa ila ni rahisi kujikata na kisu na hutumia muda kuwaandaa,kwahiyo rahisi  kuwachemsha na maganda yatatoka yenyewe.
        Ni chakula chenye thamani japokuwa ni rahisi. Kupatikana kwenye baharini na majini.
   Wanafaida za kiafya za kutosha wanacalories,Protein,Carbohydrates,fiber,fat na sodium.Ni sauce ya selenium na Vitamin B12. Na Zinc na Folate.
    Ni chakula chenye afya kwa mlaji ,na kwa familia pia.
Hufananishwa na nyama nyekundu.Na ni tamu ladha yake.
Chakula chenye afya bora ni chenye mchanganyiko wa virutubisho viloanzia 10-20% katika mlo kwa siku katika mwili wa binadamu. Na kome akiwemo.
       Kome ana fatty acids za kutosha zenye faida ambazo hujenga akili na hupunguza inflamatory conditions.
        Hujenga na kuboost immunities imara tokea kwa Vitamin na madini zinc.
         Huongeza nguvu za kiume ,kama utatumia mbichi kwa yule mwenye tatizo hili,au ya kuchemsha,ya kukaanga haishauriwi kutibu tatizo hili.

                   Jinsi ya kutengeneza mchuzi wa kome.

Baada ya kuwachemsha na kumwaga maji ukawatoa magamba.
      Unachukua mafuta ya kupikia unaweka ndani ya sufuria,kitunguu kimoja cha maji kilichokatwa,viungo vya fish masala,au kitunguu thom kijiko cha chai kimoja na tangawizi kijiko kimoja cha chai,tui zito kikombe kimoja .
Nyanya moja iloosaagwa au kukatwa vipande vidogo,na tomato paste au tomato mkebe kijiko cha chakula kimoja.
       Kaanga vitunguu viwe na rangi ya brown weka nyanya na ufunike kwa dakika kumi kisha tia viungo na tomato paste iache ichemke kwa dakika saba hadi kumi hakikisha vinaiva na kukaangika vizuri kama maji yatapungua utakua unaongeza kidogo dogo.
          Tia kome wako changanya na viungo vichanganyike vizuri kwa kukoroga,kisha tia tui na ulikoroge kwa dakika tano liive.

Nzuri kula kwa wali au kwa kutoelea chapati au mkate.
Ni tamu na nzuri kwa afya ya familia yako.

0 comments:

Post a Comment